This is featured post 1 title
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.
jiji la mwanza
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.

This is featured post 3 title
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, 30 June 2016


MBUNGE
wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) jana alijisalimisha Kituo
Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam kwa ajili ya kuhojiwa kutokana na kauli
za uchochezi alizozitoa, lakini akakosa dhamana.
Hatua
ya Lissu kukosa dhamana na kulala rumande imekuja siku moja baada ya
kuachiwa kwa dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
anakokabiliwa na mashitaka ya kuchapisha taarifa za uchochezi katika
gazeti la Mawio.
Alifika
kituoni hapo jana saa 7.38 mchana akiwa katika gari aina ya BMW lenye
namba za usajili T549 BHH na kuhojiwa kwa saa tatu mfululizo juu ya
kauli yake ya kumuita Rais John Magufuli kuwa ni dikteta ‘uchwara’,
kuandika uchochezi katika mitandao ya kijamii na kutoa kauli za kuudhi.
Kwa
mujibu wa Mwanasheria wa Lissu, John Mallya, kilichomfanya Lissu alale
rumande ni kutokana na polisi kudai kuwa amefanya uchochezi na kutumia
lugha ya kuudhi ya kusema kuna mtu anaitwa dikteta uchwara.
“Lissu
amezungumza msingi wa kwa nini amesema dikteta uchwara kwenye mahojiano
yake na amerekodiwa katika nyaraka za kipolisi na amehojiwa kwa saa
tatu kuhusu jambo hilo, na kauli aliyosema jana kutoka mahakamani,”
alisema Mallya.
Alisema
wao kama wanasheria wataendelea kumpigania Lissu na kama atafikikishwa
mahakamani leo watakuwepo kuhakikisha anapata haki zake zote za
kisheria. Mallya alidai hakuna ujumbe wowote alioandika Lissu uliokuwa
unasababisha uchochezi.
Awali,
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ambaye alikuwepo kituoni hapo,
alidai hakuna jambo baya ambalo wanaona Lissu kalizungumza, bali
alichokifanya ni kusema mtazamo wake kwa jinsi anavyoona.
Alisema
chama hicho kitaendelea kuikosoa serikali pale kitakapoona mambo
hayaendi sawa ili kuhakikisha serikali inasimama katika hali ambayo kila
mmoja ataridhishwa nayo.
Juzi
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Lissu aliachiwa kwa dhamana
katika kesi ya inayomkabili ya mashitaka ya kuchapisha taarifa za
uchochezi katika gazeti la Mawio, akijumuishwa kwenye kesi hiyo akiwa na
washtakiwa wenzake ambao ni mwandishi wa habari hizo, Jabir Idrissa,
Mhariri wa gazeti hilo, Simon Mkina na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana,
Ismail Mehboob.


RAIS Dk. John Magufuli amemtumbua mfanyabiashara mmoja maarufu Dar es Salaam, aliyebainika kufanya miamala ya fedha ya Sh milioni saba hadi nane kwa kila baada ya dakika moja.
Kutokana
na hesabu ya Sh milioni saba anayoingiza kwa dakika moja,
mfanyabiashara huyo hutengeneza Sh milioni 420 kwa kila saa moja, sawa
na Sh bilioni 5.2 kwa saa 12 na Sh trilioni 16 kwa mwezi ambazo halipi
Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).
Rais
Magufuli amesema mfanyabiashara huyo aliyebainika kuwa na makampuni
mengi, alikuwa akishirikiana na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni
nchini (BRELA) pamoja na Mamlaka ya ato Tanzania (TRA).
Mkuu
huyo wa nchi alitoa kauli hiyo Ikulu, Dar es Salaam jana, baada ya
kuwaapisha wakuu wapya wa mikoa watatu katika hafla iliyohudhuriwa pia
na wakuu wa wilaya wateule.
Alisema waligundua jipu hilo baada ya kufuatilia kwenye mapato.
“Tulikuwa
tunafuatilia kwenye ‘revenue’ (mapato), kwenye zile VAT ambazo
zinatumika ‘ku-collect revenue’ (kukusanya mapato), yupo mtu mmoja
ambaye alikuwa ametengeneza kampuni zake nyingi, alikuwa anafanya
‘transaction’ (miamala) ya fedha kila dakika moja kati ya Sh milioni
saba na nane.
“Na
hizo risiti alikuwa anaziuza kwa wafanyabiashara wengine, kwenye VAT
anatakiwa kulipia kwa asilimia 18. Wafanyabiashara wengine hao walikuwa
wanauziwa kwa asilimia tano na wakishauza bidhaa wanakwenda kuomba TRA
iwarudishie hiyo asilimia 18, kwa hiyo Serikali imekuwa ikipoteza
asilimia 18.5, ni matrilioni na matrilioni ‘of money’ (ya fedha).
“Bahati
nzuri huyo mtu yuko kwenye mikono salama, tunafuatilia namna
tutakavyorudisha hizo fedha, na huyo mtu alikuwa ana-connection kati ya
watu wa BRELA na TRA… hiyo ndiyo Tanzania.
“Najaribu
tu kutoa mfano ili katika maeneo yenu mkasimamie mapato ya Serikali,
kwa sababu tumepoteza mapato mengi kuliko tunavyofikiria, huku
Watanzania wakiteseka sana, na mambo yanayofanyika ni ya ajabu,” alisema Rais Magufuli akiwaambia wakuu hao wa mikoa na wilaya.
Pamoja
na mambo mengine, Rais Magufuli alisema mchakato wa kupata wakuu wapya
wa wilaya ulikuwa mgumu, na kwamba amewaacha wengi wa zamani kwa kuwa
hawakutimiza vigezo alivyovitaka.
“Mchakato
wa kupata ma-DC ulikuwa mgumu kwa sababu ilibidi tuangalie historia ya
kila mmoja. Tuliangalia mambo mengi sana, lakini pia tuliangalia kwa
ku-preview atatimiza haya tunayotaka kuyafanya kwa miaka mitano?
“Na
ndiyo maana mnavyoona ma-DC wa zamani waliorudi ni 39, kwa hiyo wale
101 wote hawakurudi… niseme tu ukweli kwamba hawakufikia vigezo
tulivyokuwa tunavitaka,” alisema Rais Magufuli.
Alisema katika uteuzi huo, alichukua wakurugenzi kwa kuwa walifanya vizuri katika maeneo yao waliyokuwa wakiyaongoza.
“Tulichukua
wakurugenzi walio-perform vizuri katika maeneo yao. Wapya wako
takribani 100 na waliobaki ni hao kati ya 38 na 39. Ni matumaini yangu
kwamba mtakwenda kufanya kazi na kutimiza wajibu wenu.
“DC
ni nafasi kubwa ya uongozi katika Serikali na ndiyo maana mfano mkubwa
wa DC mstaafu ni Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa), ni kwa sababu alitimiza
wajibu wake na leo yuko hapa,” alisema.
Mkuu huyo wa nchi aliwapa mikakati ya kufanya kazi wakuu hao wa wilaya kwa kutimiza dhana ya kuchapa kazi kwa niaba ya Serikali.
“Nina
matumaini makubwa mtakwenda kutimiza dhana ya kuchapa kazi kwa niaba ya
Serikali, ninyi ndio wawakilishi wetu na ndio mnawakilisha wananchi wa
maisha yote.
“Watanzania
wana matatizo na changamoto kubwa. Ni matumaini yangu kwamba
hamtaniangusha na hamtaiangusha Serikali. Nina imani mtakwenda kutatua
matatizo ya wananchi, hasa walio masikini, sitegemei wala sifikirii
kwamba mkawe chanzo cha kutengeneza matatizo,” alisema Rais Magufuli.
Kutokana
na hali hiyo, aliwataka wasimamie haki, huku wakimtanguliza Mungu
katika kufanya kazi, kusimamia maadili, kutenda haki, kutojihusisha na
rushwa, kuwatumikia Watanzania bila kubagua dini, kabila wala vyama
vyao.
“Kikubwa
mkasimamie yale tuliyoyaahidi sisi wanaCCM, kwa sababu wakati
tunazunguka tukiomba kura, yapo tuliyoyaahidi, hayo mkayatekeleze kwa
nguvu zote.
“Na
wala asitokee mtu yeyote wa kuwakwamisha kutekeleza hayo, ninyi ndio
wakuu wa wilaya na ninyi watatu ndio wakuu wa mikoa. Mna mamlaka makubwa
ya kuweka mahabusu mtu masaa 48 halafu kesho yake ukamwachia. Ila
msiende kuonea watu, mkachape kazi.
“Imani
tuliyoionyesha kwenu sisi viongozi wenu mkaionyeshe kwa Watanzania
mnaowaongoza, mkashirikiane na viongozi mtakaowaongoza, wanasema umoja
ni nguvu, utengano ni udhaifu.
“Nina
uhakika mkisimama vizuri kwa kuzingatia maadili mliyonayo, na bahati
nzuri wengi mna uzoefu katika maeneo yenu. Mkawahamasishe Watanzania
katika wilaya na mikoa yenu kufanya kazi. Watanzania wengi tumezoea
kulalamika, tunataka tupewe, lakini hatufanyi kazi. Tukawasimamie
kuchapa kazi,” alisema.
Aliwataka
wakuu hao wa wilaya ambao pia ni wenyeviti wa kamati ya ulinzi na
usalama, kukemea rushwa katika maeneo yao na kusimamia mapato ya
Serikali.
“Huwa
inatokea saa nyingine wakurugenzi kwa sababu kuna fedha nyingi
tunapelekaga kule, wanadhani ni zao wakati ni za Serikali, mkawasimamie
bila woga.
“Kupitia halmashauri zenu, mkahakikishe fedha hizo zinatumika kulingana na matakwa ya kanuni na sheria za nchi,” alisema Rais Magufuli.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Saturday, 18 June 2016


Uzimaji wa Imei bandia
ulifanyika usiku wa kuamkia jana kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA) katika simu zaidi ya 600,000 zenye Imei batili.
Kwa mujibu wa
TCRA, Imei ni namba ya kimataifa ya utambuzi wa vifaa vya kielektroniki,
ikiwamo simu. Ina tarakimu 15 ambazo ni za kipekee kwa kifaa husika na
zinatambulika kimataifa. Namba hizo hutumika kudhibiti bidhaa bandia au
simu kutumiwa na mtu mwingine.
Jana,
Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy alisema
takwimu hizo ni zile ambazo zimetokana na kazi ya kukata mawasiliano
katika simu bandia iliyofanyika kuanzia saa sita usiku mpaka saa kumi
alfajiri ya jana.
Alisisitiza kuwa mtambo huo unaendelea na kazi
kuhakikisha kuwa hata simu ambazo hazipo au hazikuwa hewani
zitakapowashwa hazitafanya kazi.
“Kazi ya kuzima simu hizo ilianza usiku
wa kumkia jana saa sita usiku na kila kampuni ya mtandao wa simu
ilipaswa kuzima simu za wateja wake ambazo ni feki na kazi ya mtambo ni
kuhakikisha simu iliyozimwa inapowekewa kadi ya mtandao mwingine
haifanyi kazi na kuhakikisha simu zote feki zitakazoingia nchini
hazifanyi kazi,” alisema Mungy.
Hata hivyo, kuna baadhi ya wamiliki wa
simu ambao walitilia shaka ufanisi wa mtambo huo kwa madai kuwa tayari
walishathibitishiwa na TCRA kwamba simu zao ni feki, lakini bado
zinafanya kazi.
“Simu yangu mimi niliangalia nikaambiwa ni feki na
niibadilishe kabla ya tarehe 16 Juni, lakini jana wamezizima feki ya
kwangu bado inafanya kazi kama kawaida napiga na kupokea simu kama
zamani,” alisema Nael Joseph.
Kuhusu suala hilo, Mungy alisema: “Hoja hizo zimejitokeza kwa wingi na wengine walifikia hatua ya kuushutumu mtambo wetu kuwa ni feki na kuwa umeshindwa kuzima simu feki ukazima orijino, lakini ukweli ni kwamba mtambo ule hauzimi kama taa au kama ule uliozima matumizi ya analojia bali unazima taratibu.
"Niweke sawa kwamba mtambo huu hauonei mtu na unazima simu zote zilizo feki.”
Mungy aliongeza kuwa wengi wamekuwa hawaelewi mantiki ya ujumbe wa uthibitisho.Alisema ujumbe unamtaka mmliki wa simu kuoanisha jina linalotajwa kama ndilo jina halisi la simu yake. “Kama jina linalotajwa na Imei linaoana na lililoandikwa kwenye simu yako, basi sio feki, lakini majina yakiwa hayafanani ndipo simu inakuwa feki,” alifafanua.
Kuhusu suala hilo, Mungy alisema: “Hoja hizo zimejitokeza kwa wingi na wengine walifikia hatua ya kuushutumu mtambo wetu kuwa ni feki na kuwa umeshindwa kuzima simu feki ukazima orijino, lakini ukweli ni kwamba mtambo ule hauzimi kama taa au kama ule uliozima matumizi ya analojia bali unazima taratibu.
"Niweke sawa kwamba mtambo huu hauonei mtu na unazima simu zote zilizo feki.”
Mungy aliongeza kuwa wengi wamekuwa hawaelewi mantiki ya ujumbe wa uthibitisho.Alisema ujumbe unamtaka mmliki wa simu kuoanisha jina linalotajwa kama ndilo jina halisi la simu yake. “Kama jina linalotajwa na Imei linaoana na lililoandikwa kwenye simu yako, basi sio feki, lakini majina yakiwa hayafanani ndipo simu inakuwa feki,” alifafanua.
Vodacom wazungumza
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Vodacom, Rosalynn Mworia alisema walipewa jukumu la kuzima simu feki za wateja wao na TCRA.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Vodacom, Rosalynn Mworia alisema walipewa jukumu la kuzima simu feki za wateja wao na TCRA.




Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema waendesha bodaboda na
abiria wasiovaa helmet watakamatwa na kushtakiwa kwa kosa la kutaka
kujiua.
Makonda
aliyemwakilisha Makamu wa Rais kwenye futari iliyoandaliwa na Benki ya
NMB kwa wateja na wadau wake juzi, alisema abiria na wapanda vyombo
hivyo wanatakiwa kuvaa helmet.
Alisema
kupanda pikipiki bila usalama ni kwamba abiria anadhamiria kujiua, kwa
sababu akipata ajali ni rahisi kupoteza maisha kwa kupiga kichwa chini.
“Nimeshawasiliana
na kamati yangu ya usalama barabarani mkoa, hili nitalisimamia
kikamilifu lazima wote wawe na helmet na wakikamatwa wote watashtakiwa,” alisema.
Mkuu
huyo wa mkoa alisema kupanda bodaboda bila kuvaa kofia hiyo, ni sawa na
mtu anayechukua vidonge na kunywa na pombe kali, ambayo matokeo yake ni
kifo.
Makonda
alisema kazi hiyo ataifanya kipindi hiki cha Mfungo wa Ramadhani ili
apate thawabu ikiwamo kuruhusu maduka makubwa kufanya kazi hadi usiku wa
manane.
Alisema
hiyo itasaidia wanaofanya kazi wakirudi nyumbani wanafuturu baadaye
wanaswali Tarawehe, hivyo wanaweza kwenda kufanya manunuzi usiku.
Alisema kitakachofanyika ni kuimarisha usalama wa raia kupitia kamati yake ya ulinzi na usalama ya mkoa.
Pia, alisema atatangaza kupiga marufuku uvutaji sigara hadharani zaidi kwenye mikusanyiko na kupambana na vijana na watu wanaojihusisha na uvutaji wa shisha (bangi).
Pia, alisema atatangaza kupiga marufuku uvutaji sigara hadharani zaidi kwenye mikusanyiko na kupambana na vijana na watu wanaojihusisha na uvutaji wa shisha (bangi).
“Mtu
asiyevuta sigara, anakerwa sana na moshi ndiye anayeathirika zaidi,
nitatangaza rasmi hivi karibuni marufuku ya kuvuta sigara, sasa watu
watafute kwa kuvutia… nitatangaza na hatua za kuchukua,” alisema.
Makonda alitumia nafasi hiyo kuwataka NMB kuchangia madawati, kwa shule za msingi na sekondari katika mkoa wake.
Makonda alitumia nafasi hiyo kuwataka NMB kuchangia madawati, kwa shule za msingi na sekondari katika mkoa wake.
Awali,
Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke Bussemaker alisema utamaduni wa
kufuturu pamoja hasa katika Afrika unadumisha amani, umoja na upendo
miongoni mwa Waislamu na watu wengine, hivyo wao wanauendeleza.


Hatima
ya shauri lililofunguliwa na Chadema dhidi ya Polisi kupinga amri ya
kupiga marufuku maandamano na mikutano ya kisiasa itajulikana Juni 21,
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza itakapotoa uamuzi kuhusu pingamizi
lililowasilishwa na upande wa utetezi kuomba litupiliwe mbali.
Jaji
Mohamed Gwae anayesikiliza shauri hilo, alifikia uamuzi huo baada ya
kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote za utetezi na mleta maombi.
Awali,
Mawakili wa utetezi, Robert Kidando na Obadia Kajungu waliomba Mahakama
kutupilia mbali maombi ya Chadema kuruhusiwa kufungua kesi
yaliyowasilishwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kwa madai
kuwa hayajakidhi mahitaji ya kisheria.
Akifafanua,
Wakili Kidando alidai mleta maombi hajataja baadhi ya vifungu muhimu
ikiwamo kifungu cha 5(1)(2), vinavyoipa Mahakama mamlaka ya kisheria
kusikiliza na kuamua maombi hayo.
Madai
hayo yalipingwa na mawakili wa Chadema; Gasper Mwanaliela na John
Mallya waliodai hoja za wajibu maombi hazina uhalali kisheria kwa sababu
hati ya maombi yaliyopo mbele ya Mahakama yamekidhi mahitaji ya
kisheria.
Wakili
Mallya alidai kisheria, hati ya maombi inapaswa kuwa na vitu vitatu
muhimu; hati ya kiapo, maelezo ya mleta maombi na ombi la shauri
kusikilizwa kama inavyoelekezwa na kifungu cha 5(3).
Wakili
Mallya aliomba Mahakama kutupilia mbali pingamizi la upande wa utetezi
na kumpa nafuu mleta maombi, kesi yake kusikilizwa na kuamuliwa.
Baada
ya kusikiliza hoja za pande zote, Jaji Gwae aliahirisha shauri hilo
hadi Juni 21, Mahakama itakapotoa uamuzi huku akiuagiza upande wa
utetezi kuwasilisha hati kinzani kujibu hoja za mleta maombi.
Katika
maombi ya msingi, Chadema inaomba Mahakama kutamka kuwa amri ya polisi
na utekelezaji wake ni batili, kwa sababu ni kinyume cha katiba na
sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992.


TANZANA
kwa sasa inajikita zaidi katika utafiti wa madini yanayohitajika zaidi
duniani yakiwemo yanayotumika kutengeneza vifaa vya simu na betri za
magari, Bunge linaloendelea na vikao vyake mjini Dodoma limeambiwa.
Aidha
katika juhudi hizo, madini aina ya helium (he) yanayotumika kwa ajili
ya mitambo ya Apollo na pia kutumika kwenye vifaa vya matibabu kama MRI
na NMR yamegundulika kuwepo nchini Tanzania.
Akijibu
maswali ya wabunge jana, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter
Muhongo, alisema kwamba baadhi ya madini kama chuma na shaba,
uhitajikaji wake duniani umepungua sana kwa sasa.
Katika
maswali yao, Mbunge wa Igunga (CCM), Dalaly Kafumu alitaka
kuthibitishiwa kuhusu uwepo wa taarifa kwamba utafiti wa madini nchini
mwetu umepungua sana.
Akijibu
swali hilo, Profesa Muhongo alitoa ufafanuzi kwamba madini yamekuwa
yakitafutwa kwa vipindi na yanapokuwa mengi, uhitajikaji wake hupungua
sambamba na utafiti.
Alifafanua kwamba katika miaka hii uhitaji wa baadhi ya madini kama shaba na chuma umepungua sana.
“Ndio
maana utaona hata uchumi wa Zambia umeyumba kwa sababu China ambayo
ndio mnunuzi mkubwa wa shaba kutoka nchini humo imepunguza mahitaji ya
madini hayo,” alisema Muhongo.
Alisema
madini yanayotengeza vifaa vya simu (rare earth mineral) na yale
yanayotengeza betri (graphite) yataendelea kutafutwa kila mara kutokana
na uhitajikaji wake na ndio maana akasema Tanzania nayo inajikita zaidi
katika kusaka madini hayo.
Alifafanua
kwamba madini hayo yanayotengeneza betri za magari yataendelea
kuhitajika sana kwa sababu ulimwengu wa sasa unajikita zaidi katika
kutengeneza magari yanayotumia umeme kwa wingi.
Kuhusu
madini ya helium ambayo huwa katika mfumo wa gesi inayopatikana katika
kina kifupi, Waziri Muhongo alifafanua kwamba utafiti ulifanywa na vyuo
vikuu vya Oxford na Durham ulithibitisha kwamba kuna madini hayo nchini.
Alifafanua
kwamba kiwango kilichogunduliwa cha madini hayo katika Ziwa Rukwa ni
mita za ujazo bilioni 52.2 na kwamba utafiti zaidi unaendelea. Kwa sasa
nchi inayozalisha kwa wingi madini hayo ni Marekani ambako hata hivyo,
Profesa Muhongo, alisema yamekuwa yakipungua siku hata siku.
Subscribe to:
Posts (Atom)