Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Mhe. Tundu Lissu alipewa dhamana saa tatu usiku wa kuamkia leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, baada ya kukana mashitaka matatu ya uchochezi aliyosomewa.
This is featured post 1 title
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.
jiji la mwanza
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.

This is featured post 3 title
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, 6 August 2016


Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Mhe. Tundu Lissu alipewa dhamana saa tatu usiku wa kuamkia leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, baada ya kukana mashitaka matatu ya uchochezi aliyosomewa.
Lissu alitimiza
masharti ya dhamana baada ya mvutano mkali wa zaidi ya saa 5 na
kujidhamini mwenyewe kwa dhamana ya shilingi milioni 10, na kesi yake
imeahirishwa hadi Agost 19, 2016.
Mapema jana
Katika Mahakama ya Hakimu MkazI Kisutu, ulinzi uliimalishwa tangu saa
mbili asubuhi ambapo askari polisi waliokuwa na silaha walikuwa
wakizunguka huku na huko kuhakikisha wafuasi wa chama hicho
hawakusanyiki katika eneo la mahakama, huku kukiwa na matarajio ya kuwa
wakati wowote atafikishwa mahakamani hapo.
Viongozi
mbalimbali wa chama hicho nao walikuwepo katika mahakama hiyo
kufuatilia kesi hiyo ya Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki.
Majira ya saa nane mchana Mhe Lissu alifikishwa mahakamani na kupandishwa kizimbani.
Akisomewa Mashataka na Wakili wa Serikali Paul Kaduche mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Cyprian Mkahe ilielezwa
kuwa Mhe Tundu Lissu alifanya makosa hayo matatu Agost 2 mwaka huu,
katika maeneo ya mahakama hiyo, kwa kutoa maneno ya uchochezi, maeneno
ya dharau katika mfumo wa utoaji haki pamoja na kuidharau mahakama ya
Kisutu.
Mshtakiwa alikana mashtaka hayo na baadaye ukatokea mvutano mkali wa kisheria juu ya uhalali wa dhamana ambapo mawakili wa serikali walikuwa wakipinga mtuhumiwa huyo kupewa dhamana.
Baada ya mvutano wa zaidi ya saa 5, kuanzia saa 10 jioni hadi saa tatu usiku, hakimu alikubali hoja za upande wa utetezi na kutoa dhamana baada ya Lissu kukamilisha masharti ya dhamana hiyo.
Mara baada ya kuchiwa, Lissu akiongozana na baadhi ya viongozi wa chama chake, aliondoka mara moja mahakamani hapo.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka


Oparesheni UKUTA Ya Chadema Yapigwa Marufuku Dar es Salaam
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda ameliagiza jeshi la polisi mkoa
wa Dar es salaam kuhakikisha kwamba sheria zinafuatwa na kusiwepo kitu
kinaitwa UKUTA ili wananchi waendelee na kazi zao kama kawaida.
Akizungumza jana na kikosi cha kutuliza ghasia katika kambi ya Ukonga Jijini Dar es salaam Mkuu wa Mkoa alisema kwa kuwa askari wanafahamu sheria wasisubiri mtu yeyote kuja kuwakumbusha juu ya jambo hilo au maelekezo mengine kwa kuwa Amiri Jeshi ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameshaagiza kinachotakiwa ni utekelezaji.
‘’Msisubiri maelekezo yoyote kutoka juu, asiwepo mtu yeyote akafunga
duka kwa sababu ya UKUTA, nyie ni matrekta hakuna UKUTA unaweza
kusimama mbele yenu, mimi kama Mkuu wa Mkoa ninaamini hatutakuwa na
vurugu kwenye Mkoa wetu na hatuwezi kuruhusu vurugu kwa kuwa tunajua
madhara ya vurugu’’ Alisema Makonda.
Aidha
kwa upande wake Kamanda wa Oparesheni Kanda Maalum ya Dar es Salaam
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Lucas Mkondya alisema
jeshi la polisi lipo vizuri na vijana wameandaliwa vizuri na
wameandaliwa kuwa tayari siku nyingi na hakuna mtu yeyote atakayethubutu
kufanya UKUTA na watakaofanya hivyo watazimwa kabla hawajafanya
chochote.
Kamada aliwataka
wananchi wote Jijini Dar es Salaam kuto jitokeza kwenye oparesheni
UKUTA kwa kuwa maandamano hayo siyo halali na watakaojitokeza watapata
matatizo yasiyowahusu.
Thursday, 30 June 2016


MBUNGE
wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) jana alijisalimisha Kituo
Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam kwa ajili ya kuhojiwa kutokana na kauli
za uchochezi alizozitoa, lakini akakosa dhamana.
Hatua
ya Lissu kukosa dhamana na kulala rumande imekuja siku moja baada ya
kuachiwa kwa dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
anakokabiliwa na mashitaka ya kuchapisha taarifa za uchochezi katika
gazeti la Mawio.
Alifika
kituoni hapo jana saa 7.38 mchana akiwa katika gari aina ya BMW lenye
namba za usajili T549 BHH na kuhojiwa kwa saa tatu mfululizo juu ya
kauli yake ya kumuita Rais John Magufuli kuwa ni dikteta ‘uchwara’,
kuandika uchochezi katika mitandao ya kijamii na kutoa kauli za kuudhi.
Kwa
mujibu wa Mwanasheria wa Lissu, John Mallya, kilichomfanya Lissu alale
rumande ni kutokana na polisi kudai kuwa amefanya uchochezi na kutumia
lugha ya kuudhi ya kusema kuna mtu anaitwa dikteta uchwara.
“Lissu
amezungumza msingi wa kwa nini amesema dikteta uchwara kwenye mahojiano
yake na amerekodiwa katika nyaraka za kipolisi na amehojiwa kwa saa
tatu kuhusu jambo hilo, na kauli aliyosema jana kutoka mahakamani,”
alisema Mallya.
Alisema
wao kama wanasheria wataendelea kumpigania Lissu na kama atafikikishwa
mahakamani leo watakuwepo kuhakikisha anapata haki zake zote za
kisheria. Mallya alidai hakuna ujumbe wowote alioandika Lissu uliokuwa
unasababisha uchochezi.
Awali,
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ambaye alikuwepo kituoni hapo,
alidai hakuna jambo baya ambalo wanaona Lissu kalizungumza, bali
alichokifanya ni kusema mtazamo wake kwa jinsi anavyoona.
Alisema
chama hicho kitaendelea kuikosoa serikali pale kitakapoona mambo
hayaendi sawa ili kuhakikisha serikali inasimama katika hali ambayo kila
mmoja ataridhishwa nayo.
Juzi
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Lissu aliachiwa kwa dhamana
katika kesi ya inayomkabili ya mashitaka ya kuchapisha taarifa za
uchochezi katika gazeti la Mawio, akijumuishwa kwenye kesi hiyo akiwa na
washtakiwa wenzake ambao ni mwandishi wa habari hizo, Jabir Idrissa,
Mhariri wa gazeti hilo, Simon Mkina na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana,
Ismail Mehboob.


RAIS Dk. John Magufuli amemtumbua mfanyabiashara mmoja maarufu Dar es Salaam, aliyebainika kufanya miamala ya fedha ya Sh milioni saba hadi nane kwa kila baada ya dakika moja.
Kutokana
na hesabu ya Sh milioni saba anayoingiza kwa dakika moja,
mfanyabiashara huyo hutengeneza Sh milioni 420 kwa kila saa moja, sawa
na Sh bilioni 5.2 kwa saa 12 na Sh trilioni 16 kwa mwezi ambazo halipi
Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).
Rais
Magufuli amesema mfanyabiashara huyo aliyebainika kuwa na makampuni
mengi, alikuwa akishirikiana na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni
nchini (BRELA) pamoja na Mamlaka ya ato Tanzania (TRA).
Mkuu
huyo wa nchi alitoa kauli hiyo Ikulu, Dar es Salaam jana, baada ya
kuwaapisha wakuu wapya wa mikoa watatu katika hafla iliyohudhuriwa pia
na wakuu wa wilaya wateule.
Alisema waligundua jipu hilo baada ya kufuatilia kwenye mapato.
“Tulikuwa
tunafuatilia kwenye ‘revenue’ (mapato), kwenye zile VAT ambazo
zinatumika ‘ku-collect revenue’ (kukusanya mapato), yupo mtu mmoja
ambaye alikuwa ametengeneza kampuni zake nyingi, alikuwa anafanya
‘transaction’ (miamala) ya fedha kila dakika moja kati ya Sh milioni
saba na nane.
“Na
hizo risiti alikuwa anaziuza kwa wafanyabiashara wengine, kwenye VAT
anatakiwa kulipia kwa asilimia 18. Wafanyabiashara wengine hao walikuwa
wanauziwa kwa asilimia tano na wakishauza bidhaa wanakwenda kuomba TRA
iwarudishie hiyo asilimia 18, kwa hiyo Serikali imekuwa ikipoteza
asilimia 18.5, ni matrilioni na matrilioni ‘of money’ (ya fedha).
“Bahati
nzuri huyo mtu yuko kwenye mikono salama, tunafuatilia namna
tutakavyorudisha hizo fedha, na huyo mtu alikuwa ana-connection kati ya
watu wa BRELA na TRA… hiyo ndiyo Tanzania.
“Najaribu
tu kutoa mfano ili katika maeneo yenu mkasimamie mapato ya Serikali,
kwa sababu tumepoteza mapato mengi kuliko tunavyofikiria, huku
Watanzania wakiteseka sana, na mambo yanayofanyika ni ya ajabu,” alisema Rais Magufuli akiwaambia wakuu hao wa mikoa na wilaya.
Pamoja
na mambo mengine, Rais Magufuli alisema mchakato wa kupata wakuu wapya
wa wilaya ulikuwa mgumu, na kwamba amewaacha wengi wa zamani kwa kuwa
hawakutimiza vigezo alivyovitaka.
“Mchakato
wa kupata ma-DC ulikuwa mgumu kwa sababu ilibidi tuangalie historia ya
kila mmoja. Tuliangalia mambo mengi sana, lakini pia tuliangalia kwa
ku-preview atatimiza haya tunayotaka kuyafanya kwa miaka mitano?
“Na
ndiyo maana mnavyoona ma-DC wa zamani waliorudi ni 39, kwa hiyo wale
101 wote hawakurudi… niseme tu ukweli kwamba hawakufikia vigezo
tulivyokuwa tunavitaka,” alisema Rais Magufuli.
Alisema katika uteuzi huo, alichukua wakurugenzi kwa kuwa walifanya vizuri katika maeneo yao waliyokuwa wakiyaongoza.
“Tulichukua
wakurugenzi walio-perform vizuri katika maeneo yao. Wapya wako
takribani 100 na waliobaki ni hao kati ya 38 na 39. Ni matumaini yangu
kwamba mtakwenda kufanya kazi na kutimiza wajibu wenu.
“DC
ni nafasi kubwa ya uongozi katika Serikali na ndiyo maana mfano mkubwa
wa DC mstaafu ni Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa), ni kwa sababu alitimiza
wajibu wake na leo yuko hapa,” alisema.
Mkuu huyo wa nchi aliwapa mikakati ya kufanya kazi wakuu hao wa wilaya kwa kutimiza dhana ya kuchapa kazi kwa niaba ya Serikali.
“Nina
matumaini makubwa mtakwenda kutimiza dhana ya kuchapa kazi kwa niaba ya
Serikali, ninyi ndio wawakilishi wetu na ndio mnawakilisha wananchi wa
maisha yote.
“Watanzania
wana matatizo na changamoto kubwa. Ni matumaini yangu kwamba
hamtaniangusha na hamtaiangusha Serikali. Nina imani mtakwenda kutatua
matatizo ya wananchi, hasa walio masikini, sitegemei wala sifikirii
kwamba mkawe chanzo cha kutengeneza matatizo,” alisema Rais Magufuli.
Kutokana
na hali hiyo, aliwataka wasimamie haki, huku wakimtanguliza Mungu
katika kufanya kazi, kusimamia maadili, kutenda haki, kutojihusisha na
rushwa, kuwatumikia Watanzania bila kubagua dini, kabila wala vyama
vyao.
“Kikubwa
mkasimamie yale tuliyoyaahidi sisi wanaCCM, kwa sababu wakati
tunazunguka tukiomba kura, yapo tuliyoyaahidi, hayo mkayatekeleze kwa
nguvu zote.
“Na
wala asitokee mtu yeyote wa kuwakwamisha kutekeleza hayo, ninyi ndio
wakuu wa wilaya na ninyi watatu ndio wakuu wa mikoa. Mna mamlaka makubwa
ya kuweka mahabusu mtu masaa 48 halafu kesho yake ukamwachia. Ila
msiende kuonea watu, mkachape kazi.
“Imani
tuliyoionyesha kwenu sisi viongozi wenu mkaionyeshe kwa Watanzania
mnaowaongoza, mkashirikiane na viongozi mtakaowaongoza, wanasema umoja
ni nguvu, utengano ni udhaifu.
“Nina
uhakika mkisimama vizuri kwa kuzingatia maadili mliyonayo, na bahati
nzuri wengi mna uzoefu katika maeneo yenu. Mkawahamasishe Watanzania
katika wilaya na mikoa yenu kufanya kazi. Watanzania wengi tumezoea
kulalamika, tunataka tupewe, lakini hatufanyi kazi. Tukawasimamie
kuchapa kazi,” alisema.
Aliwataka
wakuu hao wa wilaya ambao pia ni wenyeviti wa kamati ya ulinzi na
usalama, kukemea rushwa katika maeneo yao na kusimamia mapato ya
Serikali.
“Huwa
inatokea saa nyingine wakurugenzi kwa sababu kuna fedha nyingi
tunapelekaga kule, wanadhani ni zao wakati ni za Serikali, mkawasimamie
bila woga.
“Kupitia halmashauri zenu, mkahakikishe fedha hizo zinatumika kulingana na matakwa ya kanuni na sheria za nchi,” alisema Rais Magufuli.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Saturday, 18 June 2016


Uzimaji wa Imei bandia
ulifanyika usiku wa kuamkia jana kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA) katika simu zaidi ya 600,000 zenye Imei batili.
Kwa mujibu wa
TCRA, Imei ni namba ya kimataifa ya utambuzi wa vifaa vya kielektroniki,
ikiwamo simu. Ina tarakimu 15 ambazo ni za kipekee kwa kifaa husika na
zinatambulika kimataifa. Namba hizo hutumika kudhibiti bidhaa bandia au
simu kutumiwa na mtu mwingine.
Jana,
Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy alisema
takwimu hizo ni zile ambazo zimetokana na kazi ya kukata mawasiliano
katika simu bandia iliyofanyika kuanzia saa sita usiku mpaka saa kumi
alfajiri ya jana.
Alisisitiza kuwa mtambo huo unaendelea na kazi
kuhakikisha kuwa hata simu ambazo hazipo au hazikuwa hewani
zitakapowashwa hazitafanya kazi.
“Kazi ya kuzima simu hizo ilianza usiku
wa kumkia jana saa sita usiku na kila kampuni ya mtandao wa simu
ilipaswa kuzima simu za wateja wake ambazo ni feki na kazi ya mtambo ni
kuhakikisha simu iliyozimwa inapowekewa kadi ya mtandao mwingine
haifanyi kazi na kuhakikisha simu zote feki zitakazoingia nchini
hazifanyi kazi,” alisema Mungy.
Hata hivyo, kuna baadhi ya wamiliki wa
simu ambao walitilia shaka ufanisi wa mtambo huo kwa madai kuwa tayari
walishathibitishiwa na TCRA kwamba simu zao ni feki, lakini bado
zinafanya kazi.
“Simu yangu mimi niliangalia nikaambiwa ni feki na
niibadilishe kabla ya tarehe 16 Juni, lakini jana wamezizima feki ya
kwangu bado inafanya kazi kama kawaida napiga na kupokea simu kama
zamani,” alisema Nael Joseph.
Kuhusu suala hilo, Mungy alisema: “Hoja hizo zimejitokeza kwa wingi na wengine walifikia hatua ya kuushutumu mtambo wetu kuwa ni feki na kuwa umeshindwa kuzima simu feki ukazima orijino, lakini ukweli ni kwamba mtambo ule hauzimi kama taa au kama ule uliozima matumizi ya analojia bali unazima taratibu.
"Niweke sawa kwamba mtambo huu hauonei mtu na unazima simu zote zilizo feki.”
Mungy aliongeza kuwa wengi wamekuwa hawaelewi mantiki ya ujumbe wa uthibitisho.Alisema ujumbe unamtaka mmliki wa simu kuoanisha jina linalotajwa kama ndilo jina halisi la simu yake. “Kama jina linalotajwa na Imei linaoana na lililoandikwa kwenye simu yako, basi sio feki, lakini majina yakiwa hayafanani ndipo simu inakuwa feki,” alifafanua.
Kuhusu suala hilo, Mungy alisema: “Hoja hizo zimejitokeza kwa wingi na wengine walifikia hatua ya kuushutumu mtambo wetu kuwa ni feki na kuwa umeshindwa kuzima simu feki ukazima orijino, lakini ukweli ni kwamba mtambo ule hauzimi kama taa au kama ule uliozima matumizi ya analojia bali unazima taratibu.
"Niweke sawa kwamba mtambo huu hauonei mtu na unazima simu zote zilizo feki.”
Mungy aliongeza kuwa wengi wamekuwa hawaelewi mantiki ya ujumbe wa uthibitisho.Alisema ujumbe unamtaka mmliki wa simu kuoanisha jina linalotajwa kama ndilo jina halisi la simu yake. “Kama jina linalotajwa na Imei linaoana na lililoandikwa kwenye simu yako, basi sio feki, lakini majina yakiwa hayafanani ndipo simu inakuwa feki,” alifafanua.
Vodacom wazungumza
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Vodacom, Rosalynn Mworia alisema walipewa jukumu la kuzima simu feki za wateja wao na TCRA.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Vodacom, Rosalynn Mworia alisema walipewa jukumu la kuzima simu feki za wateja wao na TCRA.




Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema waendesha bodaboda na
abiria wasiovaa helmet watakamatwa na kushtakiwa kwa kosa la kutaka
kujiua.
Makonda
aliyemwakilisha Makamu wa Rais kwenye futari iliyoandaliwa na Benki ya
NMB kwa wateja na wadau wake juzi, alisema abiria na wapanda vyombo
hivyo wanatakiwa kuvaa helmet.
Alisema
kupanda pikipiki bila usalama ni kwamba abiria anadhamiria kujiua, kwa
sababu akipata ajali ni rahisi kupoteza maisha kwa kupiga kichwa chini.
“Nimeshawasiliana
na kamati yangu ya usalama barabarani mkoa, hili nitalisimamia
kikamilifu lazima wote wawe na helmet na wakikamatwa wote watashtakiwa,” alisema.
Mkuu
huyo wa mkoa alisema kupanda bodaboda bila kuvaa kofia hiyo, ni sawa na
mtu anayechukua vidonge na kunywa na pombe kali, ambayo matokeo yake ni
kifo.
Makonda
alisema kazi hiyo ataifanya kipindi hiki cha Mfungo wa Ramadhani ili
apate thawabu ikiwamo kuruhusu maduka makubwa kufanya kazi hadi usiku wa
manane.
Alisema
hiyo itasaidia wanaofanya kazi wakirudi nyumbani wanafuturu baadaye
wanaswali Tarawehe, hivyo wanaweza kwenda kufanya manunuzi usiku.
Alisema kitakachofanyika ni kuimarisha usalama wa raia kupitia kamati yake ya ulinzi na usalama ya mkoa.
Pia, alisema atatangaza kupiga marufuku uvutaji sigara hadharani zaidi kwenye mikusanyiko na kupambana na vijana na watu wanaojihusisha na uvutaji wa shisha (bangi).
Pia, alisema atatangaza kupiga marufuku uvutaji sigara hadharani zaidi kwenye mikusanyiko na kupambana na vijana na watu wanaojihusisha na uvutaji wa shisha (bangi).
“Mtu
asiyevuta sigara, anakerwa sana na moshi ndiye anayeathirika zaidi,
nitatangaza rasmi hivi karibuni marufuku ya kuvuta sigara, sasa watu
watafute kwa kuvutia… nitatangaza na hatua za kuchukua,” alisema.
Makonda alitumia nafasi hiyo kuwataka NMB kuchangia madawati, kwa shule za msingi na sekondari katika mkoa wake.
Makonda alitumia nafasi hiyo kuwataka NMB kuchangia madawati, kwa shule za msingi na sekondari katika mkoa wake.
Awali,
Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke Bussemaker alisema utamaduni wa
kufuturu pamoja hasa katika Afrika unadumisha amani, umoja na upendo
miongoni mwa Waislamu na watu wengine, hivyo wao wanauendeleza.


Hatima
ya shauri lililofunguliwa na Chadema dhidi ya Polisi kupinga amri ya
kupiga marufuku maandamano na mikutano ya kisiasa itajulikana Juni 21,
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza itakapotoa uamuzi kuhusu pingamizi
lililowasilishwa na upande wa utetezi kuomba litupiliwe mbali.
Jaji
Mohamed Gwae anayesikiliza shauri hilo, alifikia uamuzi huo baada ya
kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote za utetezi na mleta maombi.
Awali,
Mawakili wa utetezi, Robert Kidando na Obadia Kajungu waliomba Mahakama
kutupilia mbali maombi ya Chadema kuruhusiwa kufungua kesi
yaliyowasilishwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kwa madai
kuwa hayajakidhi mahitaji ya kisheria.
Akifafanua,
Wakili Kidando alidai mleta maombi hajataja baadhi ya vifungu muhimu
ikiwamo kifungu cha 5(1)(2), vinavyoipa Mahakama mamlaka ya kisheria
kusikiliza na kuamua maombi hayo.
Madai
hayo yalipingwa na mawakili wa Chadema; Gasper Mwanaliela na John
Mallya waliodai hoja za wajibu maombi hazina uhalali kisheria kwa sababu
hati ya maombi yaliyopo mbele ya Mahakama yamekidhi mahitaji ya
kisheria.
Wakili
Mallya alidai kisheria, hati ya maombi inapaswa kuwa na vitu vitatu
muhimu; hati ya kiapo, maelezo ya mleta maombi na ombi la shauri
kusikilizwa kama inavyoelekezwa na kifungu cha 5(3).
Wakili
Mallya aliomba Mahakama kutupilia mbali pingamizi la upande wa utetezi
na kumpa nafuu mleta maombi, kesi yake kusikilizwa na kuamuliwa.
Baada
ya kusikiliza hoja za pande zote, Jaji Gwae aliahirisha shauri hilo
hadi Juni 21, Mahakama itakapotoa uamuzi huku akiuagiza upande wa
utetezi kuwasilisha hati kinzani kujibu hoja za mleta maombi.
Katika
maombi ya msingi, Chadema inaomba Mahakama kutamka kuwa amri ya polisi
na utekelezaji wake ni batili, kwa sababu ni kinyume cha katiba na
sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992.


TANZANA
kwa sasa inajikita zaidi katika utafiti wa madini yanayohitajika zaidi
duniani yakiwemo yanayotumika kutengeneza vifaa vya simu na betri za
magari, Bunge linaloendelea na vikao vyake mjini Dodoma limeambiwa.
Aidha
katika juhudi hizo, madini aina ya helium (he) yanayotumika kwa ajili
ya mitambo ya Apollo na pia kutumika kwenye vifaa vya matibabu kama MRI
na NMR yamegundulika kuwepo nchini Tanzania.
Akijibu
maswali ya wabunge jana, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter
Muhongo, alisema kwamba baadhi ya madini kama chuma na shaba,
uhitajikaji wake duniani umepungua sana kwa sasa.
Katika
maswali yao, Mbunge wa Igunga (CCM), Dalaly Kafumu alitaka
kuthibitishiwa kuhusu uwepo wa taarifa kwamba utafiti wa madini nchini
mwetu umepungua sana.
Akijibu
swali hilo, Profesa Muhongo alitoa ufafanuzi kwamba madini yamekuwa
yakitafutwa kwa vipindi na yanapokuwa mengi, uhitajikaji wake hupungua
sambamba na utafiti.
Alifafanua kwamba katika miaka hii uhitaji wa baadhi ya madini kama shaba na chuma umepungua sana.
“Ndio
maana utaona hata uchumi wa Zambia umeyumba kwa sababu China ambayo
ndio mnunuzi mkubwa wa shaba kutoka nchini humo imepunguza mahitaji ya
madini hayo,” alisema Muhongo.
Alisema
madini yanayotengeza vifaa vya simu (rare earth mineral) na yale
yanayotengeza betri (graphite) yataendelea kutafutwa kila mara kutokana
na uhitajikaji wake na ndio maana akasema Tanzania nayo inajikita zaidi
katika kusaka madini hayo.
Alifafanua
kwamba madini hayo yanayotengeneza betri za magari yataendelea
kuhitajika sana kwa sababu ulimwengu wa sasa unajikita zaidi katika
kutengeneza magari yanayotumia umeme kwa wingi.
Kuhusu
madini ya helium ambayo huwa katika mfumo wa gesi inayopatikana katika
kina kifupi, Waziri Muhongo alifafanua kwamba utafiti ulifanywa na vyuo
vikuu vya Oxford na Durham ulithibitisha kwamba kuna madini hayo nchini.
Alifafanua
kwamba kiwango kilichogunduliwa cha madini hayo katika Ziwa Rukwa ni
mita za ujazo bilioni 52.2 na kwamba utafiti zaidi unaendelea. Kwa sasa
nchi inayozalisha kwa wingi madini hayo ni Marekani ambako hata hivyo,
Profesa Muhongo, alisema yamekuwa yakipungua siku hata siku.
Wednesday, 20 April 2016


Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ameahirisha kwa muda kwenda
bungeni mjini Dodoma, kufuatia kuungua moto kwa mabweni ya Shule ya
Sekondari Bwilingu.
Akizungumza shuleni hapo juzi jioni,
Ridhiwani alisema katika vipaumbele vyake elimu ni mojawapo, hivyo
hawezi kuondoka na kuwaacha wanafunzi waliounguliwa vifaa wakishika tama
na wengine kushindwa kuhudhuria darasani kwa kukosa nguo na madaftari.
Alisema
moto ni kitu cha dharura na kwa kutambua hivyo, amewasiliana na wadau
mbalimbali na wahisani ambao wameamua kulivunja jengo lililoungua na
kulijenga upya, kazi iliyoanza jana.
Ridhiwani alisema
wamechangia misaada mbalimbali ikiwamo magodoro, vitanda, nguo, vyombo,
madaftari, sabuni, vyandarua, mafuta, dawa ya mswaki na miswaki kwa
wanafunzi hao.
“Unajua moto ulitokea usiku, sasa muda huo ina
maana hao wanafunzi 65 walikuwa na kalamu moja na daftari moja au mawili
wanajisomea darasani, vingine vyote vilikuwa mabwenini na vimeungua,”
alisema.
“Kwa hiyo nimeona bora nishirikiane na wenzangu kutatua
hili na nimetoa tayari magodoro 70 na mashuka 140 na nguo kadhaa waanze
navyo, huku vingine vikifuata baadaye.”
Mkuu wa sekondari hiyo,
Emmanuel Kahabi alisema pamoja na kupata maafa hayo, jana wanafunzi
waliendelea na masomo kama kawaida kwa kuwa baada ya tukio, wadau
mbalimbali walikutana na kuanza kutoa misaada.
Moto huo ulitokea
Jumapili usiku na kuteketeza vifaa na mali zote zilizokuwa ndani wakati
wanafunzi wakiwa kwenye masomo ya usiku madarasani.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Thursday, 7 April 2016



Siku 155 baada ya Dk John Magufuli kuapishwa kuwa Rais, aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema katika uchaguzi huo, Edward Lowassa ametaja mambo matano yanayomfanya autilie shaka mustakabali wa Taifa chini ya uongozi wa Rais huyo wa Awamu ya Tano.
Akizungumza na wanazuoni wa ndani na nje ya nchi wakiongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Profesa Rwekaza Mukandala nyumbani kwake Masaki Dar es Salaam, Lowassa alisema: “Hali ya siasa nchini ni ya hamasa lakini isiyo na msingi endelevu.”
Lowassa, ambaye alishika nafasi ya pili katika uchaguzi huo baada ya kupata kura milioni 6.07 sawa na asilimia 39.97 aliyataja mambo hayo kuwa ni Rais kugawa fedha wakati chombo cha kufanya hivyo kipo, watumishi kuachishwa kazi, upitishaji mizigo Bandari ya Dar es Salaam kushuka, nchi kunyimwa misaada na ugumu wa maisha unaowakabili wananchi hivi sasa.
Katika uchaguzi huo, Rais Magufuli alipata kura milioni 8.8 sawa na asilimia 58.47 na kumshinda Lowassa ambaye alikuwa amejiunga Chadema Julai mwaka jana akitokea CCM ambako jina lake lilikatwa katika mchakato wa chama hicho kupata mgombea urais.
Tangu aingie Ikulu, Rais Magufuli amekuwa akichukua hatua mbalimbali za kutengua uteuzi au kuwasimamisha kazi watendaji mbalimbali wa Serikali, kufuta maadhimisho ya sherehe mbalimbali na kuagiza fedha zitumike kutekeleza miradi mingine huku akiwabana wafanyabiashara kulipa kodi.
Uamuzi wake huo unaofanywa pia na mawaziri wake umekuwa ukipongezwa na kukosolewa na watu wa kada mbalimbali na jana Lowassa alikuwa miongoni mwa wakosoaji hao ikiwa ni mara yake ya pili tangu Dk Magufuli aingie madarakani.
Mara ya kwanza, Lowassa alikosoa sera ya elimu bure, alipoitofautisha na ile aliyokuwa ameahidi ya kuanzia awali hadi chuo kikuu na kuhoji iwapo Rais Magufuli mbali na ada angefuta pia michango mingine, jambo ambalo lilifanyiwa kazi.
Alipoulizwa kuhusu mazungumzo hayo, Profesa Mukandala alisema: “Tunafanya utafiti kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa, uchumi, utawala bora na ushindani wa siasa na tunazungumza na watu kutoka vyama mbalimbali na viongozi wa Serikali.”
Waziri wa Habari, Nape Nnauye alipoulizwa kuhusu kauli hiyo ya Lowassa alisema waziri mkuu huyo wa zamani anapingana na viongozi wa Chadema wanaokiri wazi kuwa Rais Magufuli anatekeleza sera na mikakati ya upinzani.
Kauli ya Lowassa
Taarifa iliyotolewa jana na ofisi ya Lowassa ilisema mwanasiasa huyo aliwaeleza wanazuoni hao kuwa; “hali ya siasa hivi sasa ni ya hamasa kutokana na Serikali mpya na ‘style’ mpya. Kwa kipindi kifupi atakuwa lakini hakuna mafanikio ya kiuchumi mbele ya safari.”
Alisema Rais amekuwa akigawa fedha wakati chombo cha kufanya hivyo kipo ambacho ni Bunge.
Rais Magufuli amekuwa na utaratibu kuidhinisha fedha zilizotengwa kwa ajili ya sherehe mbalimbali kutumika katika shu ghuli nyingine. Juzi, aliagiza Sh2 bilioni zilizokuwa zitumike katika Siku ya Muungano zitumike kupanua barabara inayokwenda Uwanja wa Ndege wa Mwanza.
Pia, amewahi kuamuru Sh4 bilioni za Siku ya Uhuru kupanua Barabara ya Morocco – Mwenge, Dar es Salaam.
Aliagiza pia fedha za maadhimisho ya siku ya Ukimwi kutumika kununua vifaatiba na Sh225 milioni zilizotengwa kwa ajili ya hafla ya uzinduzi wa Bunge zilinunulia vitanda Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Lowassa pia alieleza kusononeshwa na hali ngumu ya maisha na idadi kubwa ya watu kuachishwa kazi.
“Nasononeshwa ninapoona watu wanaachishwa kazi na mashirika mbalimbali kwa sababu ya hali ngumu ya uendeshaji wa mashirika hayo.
“Bandarini sasa hivi nasikia uingizaji mizigo umeshuka kwa asilimia 50, kampuni nyingi za mizigo zimefunga shughuli zake na pale kulikuwa na vijana wetu wengi wana ajira, sasa hivi wako mitaani, hali inatisha maisha ya mwananchi yanazidi kuwa magumu,” alisema.
Lowassa aligusia uamuzi wa Marekani kupitia bodi yake ya Changamoto za Milenia (MCC) kusitisha msaada wa zaidi ya Sh1 trilioni.
“Ni pigo kwa mustakabali wa uchumi. Halafu tunasema tunataka nchi ya viwanda, hela tutatoa wapi kama si hawa wafadhili wa ndani na nje kusaidia katika hilo?” alihoji.
Lowassa ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema alisema: “Hawa wafadhili siyo watu wa kuwabeza wataturudisha nyuma. Jakaya (Kikwete- Rais mstaafu wa Awamu ya Nne) kwa kiasi kidogo alijitahidi kuvutia wawekezaji, japo kulikuwa na uzembe na ufisadi katika kuwasimamia.
“Hapa kinachotakiwa ni kufanya mabadiliko katika mfumo na kuufanya kuwa endelevu,” alisema.
Alisema si kweli kuwa kila mtu katika Serikali ya Awamu ya Nne alikuwa mla rushwa huku akikiri kuwa mfumo wa Serikali hiyo ulikuwa mbovu na wa kifisadi.
Aliwaeleza wanazuoni hao kuwa: “Uchaguzi ule tulishinda (upinzani) na kila mtu anajua hivyo. Hata Magufuli anajua hilo...,” alisema.
Akizungumzia mikakati ya upinzani, Lowassa alisema wamejipanga kuhakikisha hawaporwi tena ushindi na kusisitiza kuwa joto la kutaka mabadiliko bado ni kubwa na Watanzania wameichoka CCM.
Kauli na Nape
Akijibu hoja zilizotolewa na Lowassa, Nape alisema, “Anajichanganya tu, maana Mbowe (Freeman – Mwenyekiti wa Chadema) amenukuliwa akisema Rais Magufuli anaiga kila kitu cha Chadema, sasa yeye (Lowassa) anaposema hayo maana yake haelewani na Mbowe.”
Alisema litakuwa jambo la ajabu kama Lowassa atakubali kila jambo linalofanywa na Serikali iliyopo madarakani kwa kuwa ndivyo alivyo.
“Katika Uchaguzi Mkuu Lowassa hakuchaguliwa na wananchi ila Magufuli alichaguliwa kwa sababu wananchi walifurahishwa na sera zake, hivyo amuache mwenzake atekeleze ahadi zake kwa wananchi,” alisema Nape.
“Kwanza Lowassa amekuwa mtetezi wa wezi, mafisadi na wala rushwa. Unawateteaje watu wa aina hii wanapofukuzwa kazi. Amebanwa tu na kwake kazi inayofanywa na Magufuli inampa maumivu.”
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven amemwagiza Kamanda wa Polisi mkoa huo, Jacob Mwaruanda kuwasaka na kuwakamata watumishi hewa 18 waliobainika katika uhakiki uliofanyika katika halmashauri zote mkoani humo hivi karibuni.
Pia ameagiza fedha hizo zilizolipwa kwa watumishi hao hewa na kuiingizia hasara kubwa Serikali zirudishwe mara moja.
Akifafanua alisema katika uhakiki huo, watumishi hewa tisa walibainika katika wilaya ya Nkasi, wanane katika Manispaa ya Sumbawanga na mmoja wilaya ya Sumbawanga wakati Kalambo ikiwa haina mtumishi hewa.
Uhakiki huo unatokana na maagizo aliyotoa Rais John Magufuli baada ya kuwaapisha wakuu wa mikoa aliowateua, aliwaambia wakafanye kazi ya kutatua kero za wananchi na sio kwenda kufanya siasa.
Pia Rais Magufuli aliwapa wakurugenzi wa halmashauri siku 15 wawatoe katika orodha ya malipo ya mshahara wafanyakazi hewa wote katika halmashauri zote nchini.
Zelothe alitoa agizo hilo jana katika kikao maalumu cha kufahamiana kilichojumuisha wazee , viongozi wa dini , watendaji wa umma na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo kilichofanyika mjini hapa.
Alisisitiza kuwa hajaridhishwa na uhakiki huo, hivyo akaagiza halmashuri zote kurudia upya uhakiki wa watumishi.
Alisisitiza kuwa hajaridhishwa na uhakiki huo, hivyo akaagiza halmashuri zote kurudia upya uhakiki wa watumishi.
“Siku ile ile nilipoapishwa kabla sijavuka geti kutoka nje ya Ikulu nilipiga simu na kuagiza halmashauri zote (Manispaa, Nkasi, Kalambo na Sumbawanga) kuanza uhakiki mara moja wasinisubiri hadi niripoti mkoani hapa,” alieleza.
Aliongeza kuwa aliporudi mkoani humo na kuripoti kazini katika siku yake ya kwanza ofisini alikabidhiwa kitabu chenye orodha ya watumishi wa umma wa halmashauri zote akielezwa kuwa hakuna mtumishi hewa katika mkoa wa Rukwa.
“Sikukubaliana nao nilikataa, nikaagiza ufanyike uhakiki mara moja ndipo wamepatikana watumishi hewa 18 na watumishi wengine 137 wapowapo tu wakiwa na taarifa zinazotia mashaka. Wote wamebainika kwenye hicho kitabu nilichokabidhiwa kikionesha hakuna mtumishi hewa,” alisisitiza.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )



Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa nchini (Alat), wanaotokana na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wamesusia uchaguzi kwa madai ya kuminywa kwa demokrasia.
Mkutano huo uliofanyika jana katika ukumbi mpya wa CCM mjini Dodoma, wajumbe wake ni wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri zote, mameya wa miji na majiji na mbunge mmoja kutoka kila mkoa wa Tanzania Bara.
Nafasi zilizokuwa zikigombewa ni mwenyekiti, makamu wake na wajumbe 16 wa kamati ya utendaji.
Awali, Mwanasheria wa Alat, Cleofas Manyangu aliwataja waliochukua na kurejesha fomu za kugombea uenyekiti ni Gulam Mukadam (Meya wa Shinyanga), Murshid Ngeze (Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bukoba Vijijini), Chief Kalumuna (Meya wa Bukoba Mjini) na Isaya Charles (Meya wa Jiji la Dar es Salaam).
Hata hivyo, alisema waliokidhi vigezo kwa mujibu wa Katiba ya Alat, kanuni za kudumu na mwongozo ni Mukadam na Ngeze wote kutoka CCM na waliosalia wa Ukawa hawakukidhi.
Alisema Charles na Kalumuna walishindwa kurejesha fomu katika muda uliowekwa wa saa 6.00 mchana siku moja kabla ya uchaguzi na pia hawakupata wadhamini 10 kutoka kanda tano za Alat Taifa.
Kutokana na kauli ya mwanasheria huyo, mwenyekiti wa muda wa mkutano huo ambaye pia ni Meya wa Manispaa ya Dodoma, Jaffar Mwanyemba alitangaza kuwa wagombea katika uchaguzi huo ni wawili.
Kauli hiyo ilibadilisha hali katika ukumbi, huku wajumbe wa Ukawa wakitaka wagombea wote waruhusiwe kuingia katika kinyang’anyiro hicho.
Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro aliomba wagombea hao waruhusiwe kwa kuwa maandalizi ya uchaguzi yalikiuka mwongozo, hali ambayo ilifanya baadhi yao kutokidhi vigezo.
Alisema taarifa ya mkutano huo ilitakiwa kuwafikia siku zisizopungua 28 kabla ya uchaguzi, lakini wengi wao walipata barua hizo chini ya muda huo.
Akijibu hoja hizo, Manyangu alisema taarifa za mkutano huo kwa mara ya kwanza zilipelekwa kwenye halmashauri Novemba 2, mwaka jana.
“Tatizo lililotokea ni baadhi ya halmashauri kuchelewa kukamilisha uchaguzi, hali iliyosababisha mkutano kuahirishwa mara mbili,” alisema.
Baada ya hoja hizo, wajumbe wote wanaotokana na Ukawa walitoka nje ya ukumbi, huku wakiahidi kufanya kazi na Serikali Kuu pekee.
Akizungumza nje ya ukumbi, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Charles alisema kutokana na kuchelewa kwa uchaguzi jijini humo hakupata taarifa mapema kuhusu mkutano na uchaguzi huo.
Hata hivyo, Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe na meya wa Manispaa ya Kigoma walishiriki uchaguzi kama kawaida.
“Mimi sijui chochote. Sijui wametoka kwa sababu gani maana nimefika hapa nikiwa nimechelewa,” alisema Zitto.
Katika uchaguzi huo, Mukadam alichaguliwa kuwa mwenyekiti kwa kura 179 kati ya 276 na makamu wake ni Stephen Muhapa aliyepata kura 152 kati ya 272.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Subscribe to:
Posts (Atom)