Wednesday, 20 April 2016


Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ameahirisha kwa muda kwenda bungeni mjini Dodoma, kufuatia kuungua moto kwa mabweni ya Shule ya Sekondari Bwilingu.

Akizungumza shuleni hapo juzi jioni, Ridhiwani alisema katika vipaumbele vyake elimu ni mojawapo, hivyo hawezi kuondoka na kuwaacha wanafunzi waliounguliwa vifaa wakishika tama na wengine kushindwa kuhudhuria darasani kwa kukosa nguo na madaftari.

Alisema moto ni kitu cha dharura na kwa kutambua hivyo, amewasiliana na wadau mbalimbali na wahisani ambao wameamua kulivunja jengo lililoungua na kulijenga upya, kazi iliyoanza jana.

Ridhiwani alisema wamechangia misaada mbalimbali ikiwamo magodoro, vitanda, nguo, vyombo, madaftari, sabuni, vyandarua, mafuta, dawa ya mswaki na miswaki kwa wanafunzi hao.

“Unajua moto ulitokea usiku, sasa muda huo ina maana hao wanafunzi 65 walikuwa na kalamu moja na daftari moja au mawili wanajisomea darasani, vingine vyote vilikuwa mabwenini na vimeungua,” alisema.

“Kwa hiyo nimeona bora nishirikiane na wenzangu kutatua hili na nimetoa tayari magodoro 70 na mashuka 140 na nguo kadhaa waanze navyo, huku vingine vikifuata baadaye.”

Mkuu wa sekondari hiyo, Emmanuel Kahabi alisema pamoja na kupata maafa hayo, jana wanafunzi waliendelea na masomo kama kawaida kwa kuwa baada ya tukio, wadau mbalimbali walikutana na kuanza kutoa misaada.
 Moto huo ulitokea Jumapili usiku na kuteketeza vifaa na mali zote zilizokuwa ndani wakati wanafunzi wakiwa kwenye masomo ya usiku madarasani.
<a href='http://mpekuzihosting.com/ads/www/delivery/ck.php?n=a5fa0220&cb=INSERT_RANDOM_NUMBER_HERE' target='_blank'><img alt='' border='0' src='http://mpekuzihosting.com/ads/www/delivery/avw.php?zoneid=3&cb=INSERT_RANDOM_NUMBER_HERE&n=a5fa0220'/></a> ;
==

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Thursday, 7 April 2016



Siku 155 baada ya Dk John Magufuli kuapishwa kuwa Rais, aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema katika uchaguzi huo, Edward Lowassa ametaja mambo matano yanayomfanya autilie shaka mustakabali wa Taifa chini ya uongozi wa Rais huyo wa Awamu ya Tano.

Akizungumza na wanazuoni wa ndani na nje ya nchi wakiongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Profesa Rwekaza Mukandala nyumbani kwake Masaki Dar es Salaam, Lowassa alisema: “Hali ya siasa nchini ni ya hamasa lakini isiyo na msingi endelevu.

Lowassa, ambaye alishika nafasi ya pili katika uchaguzi huo baada ya kupata kura milioni 6.07 sawa na asilimia 39.97 aliyataja mambo hayo kuwa ni Rais kugawa fedha wakati chombo cha kufanya hivyo kipo, watumishi kuachishwa kazi, upitishaji mizigo Bandari ya Dar es Salaam kushuka, nchi kunyimwa misaada na ugumu wa maisha unaowakabili wananchi hivi sasa.

Katika uchaguzi huo, Rais Magufuli alipata kura milioni 8.8 sawa na asilimia 58.47 na kumshinda Lowassa ambaye alikuwa amejiunga Chadema Julai mwaka jana akitokea CCM ambako jina lake lilikatwa katika mchakato wa chama hicho kupata mgombea urais.

Tangu aingie Ikulu, Rais Magufuli amekuwa akichukua hatua mbalimbali za kutengua uteuzi au kuwasimamisha kazi watendaji mbalimbali wa Serikali, kufuta maadhimisho ya sherehe mbalimbali na kuagiza fedha zitumike kutekeleza miradi mingine huku akiwabana wafanyabiashara kulipa kodi.

Uamuzi wake huo unaofanywa pia na mawaziri wake umekuwa ukipongezwa na kukosolewa na watu wa kada mbalimbali na jana Lowassa alikuwa miongoni mwa wakosoaji hao ikiwa ni mara yake ya pili tangu Dk Magufuli aingie madarakani.

Mara ya kwanza, Lowassa alikosoa sera ya elimu bure, alipoitofautisha na ile aliyokuwa ameahidi ya kuanzia awali hadi chuo kikuu na kuhoji iwapo Rais Magufuli mbali na ada angefuta pia michango mingine, jambo ambalo lilifanyiwa kazi.

Alipoulizwa kuhusu mazungumzo hayo, Profesa Mukandala alisema: “Tunafanya utafiti kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa, uchumi, utawala bora na ushindani wa siasa na tunazungumza na watu kutoka vyama mbalimbali na viongozi wa Serikali.”

Waziri wa Habari, Nape Nnauye alipoulizwa kuhusu kauli hiyo ya Lowassa alisema waziri mkuu huyo wa zamani anapingana na viongozi wa Chadema wanaokiri wazi kuwa Rais Magufuli anatekeleza sera na mikakati ya upinzani. 

Kauli ya Lowassa 
Taarifa iliyotolewa jana na ofisi ya Lowassa ilisema mwanasiasa huyo aliwaeleza wanazuoni hao kuwa; “hali ya siasa hivi sasa ni ya hamasa kutokana na Serikali mpya na ‘style’ mpya. Kwa kipindi kifupi atakuwa lakini hakuna mafanikio ya kiuchumi mbele ya safari.”

Alisema Rais amekuwa akigawa fedha wakati chombo cha kufanya hivyo kipo ambacho ni Bunge.

Rais Magufuli amekuwa na utaratibu kuidhinisha fedha zilizotengwa kwa ajili ya sherehe mbalimbali kutumika katika shu ghuli nyingine. Juzi, aliagiza Sh2 bilioni zilizokuwa zitumike katika Siku ya Muungano zitumike kupanua barabara inayokwenda Uwanja wa Ndege wa Mwanza.

Pia, amewahi kuamuru Sh4 bilioni za Siku ya Uhuru kupanua Barabara ya Morocco – Mwenge, Dar es Salaam. 

Aliagiza pia fedha za maadhimisho ya siku ya Ukimwi kutumika kununua vifaatiba na Sh225 milioni zilizotengwa kwa ajili ya hafla ya uzinduzi wa Bunge zilinunulia vitanda Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Lowassa pia alieleza kusononeshwa na hali ngumu ya maisha na idadi kubwa ya watu kuachishwa kazi.

“Nasononeshwa ninapoona watu wanaachishwa kazi na mashirika mbalimbali kwa sababu ya hali ngumu ya uendeshaji wa mashirika hayo.

“Bandarini sasa hivi nasikia uingizaji mizigo umeshuka kwa asilimia 50, kampuni nyingi za mizigo zimefunga shughuli zake na pale kulikuwa na vijana wetu wengi wana ajira, sasa hivi wako mitaani, hali inatisha maisha ya mwananchi yanazidi kuwa magumu,” alisema.

Lowassa aligusia uamuzi wa Marekani kupitia bodi yake ya Changamoto za Milenia (MCC) kusitisha msaada wa zaidi ya Sh1 trilioni.

“Ni pigo kwa mustakabali wa uchumi. Halafu tunasema tunataka nchi ya viwanda, hela tutatoa wapi kama si hawa wafadhili wa ndani na nje kusaidia katika hilo?” alihoji.

Lowassa ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema alisema: “Hawa wafadhili siyo watu wa kuwabeza wataturudisha nyuma. Jakaya (Kikwete- Rais mstaafu wa Awamu ya Nne) kwa kiasi kidogo alijitahidi kuvutia wawekezaji, japo kulikuwa na uzembe na ufisadi katika kuwasimamia.

“Hapa kinachotakiwa ni kufanya mabadiliko katika mfumo na kuufanya kuwa endelevu,” alisema.

Alisema si kweli kuwa kila mtu katika Serikali ya Awamu ya Nne alikuwa mla rushwa huku akikiri kuwa mfumo wa Serikali hiyo ulikuwa mbovu na wa kifisadi.

Aliwaeleza wanazuoni hao kuwa: “Uchaguzi ule tulishinda (upinzani) na kila mtu anajua hivyo. Hata Magufuli anajua hilo...,” alisema.

Akizungumzia mikakati ya upinzani, Lowassa alisema wamejipanga kuhakikisha hawaporwi tena ushindi na kusisitiza kuwa joto la kutaka mabadiliko bado ni kubwa na Watanzania wameichoka CCM.

Kauli na Nape 
Akijibu hoja zilizotolewa na Lowassa, Nape alisema, “Anajichanganya tu, maana Mbowe (Freeman – Mwenyekiti wa Chadema) amenukuliwa akisema Rais Magufuli anaiga kila kitu cha Chadema, sasa yeye (Lowassa) anaposema hayo maana yake haelewani na Mbowe.”

Alisema litakuwa jambo la ajabu kama Lowassa atakubali kila jambo linalofanywa na Serikali iliyopo madarakani kwa kuwa ndivyo alivyo.

“Katika Uchaguzi Mkuu Lowassa hakuchaguliwa na wananchi ila Magufuli alichaguliwa kwa sababu wananchi walifurahishwa na sera zake, hivyo amuache mwenzake atekeleze ahadi zake kwa wananchi,” alisema Nape.

“Kwanza Lowassa amekuwa mtetezi wa wezi, mafisadi na wala rushwa. Unawateteaje watu wa aina hii wanapofukuzwa kazi. Amebanwa tu na kwake kazi inayofanywa na Magufuli inampa maumivu.”
;
==


Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven
 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven amemwagiza Kamanda wa Polisi mkoa huo, Jacob Mwaruanda kuwasaka na kuwakamata watumishi hewa 18 waliobainika katika uhakiki uliofanyika katika halmashauri zote mkoani humo hivi karibuni.

Pia ameagiza fedha hizo zilizolipwa kwa watumishi hao hewa na kuiingizia hasara kubwa Serikali zirudishwe mara moja.

Akifafanua alisema katika uhakiki huo, watumishi hewa tisa walibainika katika wilaya ya Nkasi, wanane katika Manispaa ya Sumbawanga na mmoja wilaya ya Sumbawanga wakati Kalambo ikiwa haina mtumishi hewa.

Uhakiki huo unatokana na maagizo aliyotoa Rais John Magufuli baada ya kuwaapisha wakuu wa mikoa aliowateua, aliwaambia wakafanye kazi ya kutatua kero za wananchi na sio kwenda kufanya siasa.

Pia Rais Magufuli aliwapa wakurugenzi wa halmashauri siku 15 wawatoe katika orodha ya malipo ya mshahara wafanyakazi hewa wote katika halmashauri zote nchini.

Zelothe alitoa agizo hilo jana katika kikao maalumu cha kufahamiana kilichojumuisha wazee , viongozi wa dini , watendaji wa umma na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo kilichofanyika mjini hapa.

Alisisitiza kuwa hajaridhishwa na uhakiki huo, hivyo akaagiza halmashuri zote kurudia upya uhakiki wa watumishi.

“Siku ile ile nilipoapishwa kabla sijavuka geti kutoka nje ya Ikulu nilipiga simu na kuagiza halmashauri zote (Manispaa, Nkasi, Kalambo na Sumbawanga) kuanza uhakiki mara moja wasinisubiri hadi niripoti mkoani hapa,” alieleza.

Aliongeza kuwa aliporudi mkoani humo na kuripoti kazini katika siku yake ya kwanza ofisini alikabidhiwa kitabu chenye orodha ya watumishi wa umma wa halmashauri zote akielezwa kuwa hakuna mtumishi hewa katika mkoa wa Rukwa.

“Sikukubaliana nao nilikataa, nikaagiza ufanyike uhakiki mara moja ndipo wamepatikana watumishi hewa 18 na watumishi wengine 137 wapowapo tu wakiwa na taarifa zinazotia mashaka. Wote wamebainika kwenye hicho kitabu nilichokabidhiwa kikionesha hakuna mtumishi hewa,” alisisitiza.
;
==


Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )

Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa nchini (Alat), wanaotokana na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wamesusia uchaguzi kwa madai ya kuminywa kwa demokrasia.

Mkutano huo uliofanyika jana katika ukumbi mpya wa CCM mjini Dodoma, wajumbe wake ni wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri zote, mameya wa miji na majiji na mbunge mmoja kutoka kila mkoa wa Tanzania Bara.

Nafasi zilizokuwa zikigombewa ni mwenyekiti, makamu wake na wajumbe 16 wa kamati ya utendaji.

Awali, Mwanasheria wa Alat, Cleofas Manyangu aliwataja waliochukua na kurejesha fomu za kugombea uenyekiti ni Gulam Mukadam (Meya wa Shinyanga), Murshid Ngeze (Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bukoba Vijijini), Chief Kalumuna (Meya wa Bukoba Mjini) na Isaya Charles (Meya wa Jiji la Dar es Salaam).

Hata hivyo, alisema waliokidhi vigezo kwa mujibu wa Katiba ya Alat, kanuni za kudumu na mwongozo ni Mukadam na Ngeze wote kutoka CCM na waliosalia wa Ukawa hawakukidhi.

Alisema Charles na Kalumuna walishindwa kurejesha fomu katika muda uliowekwa wa saa 6.00 mchana siku moja kabla ya uchaguzi na pia hawakupata wadhamini 10 kutoka kanda tano za Alat Taifa.

Kutokana na kauli ya mwanasheria huyo, mwenyekiti wa muda wa mkutano huo ambaye pia ni Meya wa Manispaa ya Dodoma, Jaffar Mwanyemba alitangaza kuwa wagombea katika uchaguzi huo ni wawili.

Kauli hiyo ilibadilisha hali katika ukumbi, huku wajumbe wa Ukawa wakitaka wagombea wote waruhusiwe kuingia katika kinyang’anyiro hicho.

Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro aliomba wagombea hao waruhusiwe kwa kuwa maandalizi ya uchaguzi yalikiuka mwongozo, hali ambayo ilifanya baadhi yao kutokidhi vigezo.

Alisema taarifa ya mkutano huo ilitakiwa kuwafikia siku zisizopungua 28 kabla ya uchaguzi, lakini wengi wao walipata barua hizo chini ya muda huo.

Akijibu hoja hizo, Manyangu alisema taarifa za mkutano huo kwa mara ya kwanza zilipelekwa kwenye halmashauri Novemba 2, mwaka jana.

“Tatizo lililotokea ni baadhi ya halmashauri kuchelewa kukamilisha uchaguzi, hali iliyosababisha mkutano kuahirishwa mara mbili,” alisema.

Baada ya hoja hizo, wajumbe wote wanaotokana na Ukawa walitoka nje ya ukumbi, huku wakiahidi kufanya kazi na Serikali Kuu pekee.

Akizungumza nje ya ukumbi, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Charles alisema kutokana na kuchelewa kwa uchaguzi jijini humo hakupata taarifa mapema kuhusu mkutano na uchaguzi huo.

Hata hivyo, Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe na meya wa Manispaa ya Kigoma walishiriki uchaguzi kama kawaida.

“Mimi sijui chochote. Sijui wametoka kwa sababu gani maana nimefika hapa nikiwa nimechelewa,” alisema Zitto.

Katika uchaguzi huo, Mukadam alichaguliwa kuwa mwenyekiti kwa kura 179 kati ya 276 na makamu wake ni Stephen Muhapa aliyepata kura 152 kati ya 272.
;
==


Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Wednesday, 6 April 2016


Rais Magufuli Kagame Wazindua Daraja la Rusumo Rwanda

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Rwanda, Paul Kagame wakifurahia mara baada ya kuzindua rasmi daraja la kimataifa la Rusumo na Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) cha Rusumo.
Rais Magufuli na Rais Kagame wakikata utepe kwa pamoja kuashiria uzinduzi rasmi wa daraja la kimataifa la Rusumo na Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) cha Rusumo.
 Muonekano wa sehemu ya Daraja hilo la Rusumo
 Jiwe la msingi lililowekwa baada ya uzinduzi wa daraja hilo
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame wakipita kwenye Daraja hilo la Rusumo mara baada ya uzinduzi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame wakikata utepe kwa pamoja kuashiria uzinduzi  wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) cha Rusumo. Tukio hilo limehudhuriwa na viongozi wa ngazi za juu serkalini kutoka Nchi zote mbili, Mabalozi, na Viongozi wa Taasisi mbambali za Kitaifa na Kimataifa.
 Picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa huo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame leo wamezindua rasmi Daraja la Kimataifa la Rusumo na Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) cha Rusumo. Daraja hilo linakatisha mto Kagera na kuunganisha nchi za Rwanda na Tanzania.
Tukio la uzinduzi huo lililohudhuriwa na viongozi wa ngazi za juu serkalini kutoka Nchi zote mbili, Mabalozi, na Viongozi wa Taasisi mbambali za Kitaifa na Kimataifa.
Ujenzi wa Daraja la Kimataifa la Rusumo na Kituo cha huduma Pamoja Mpakani Rusumo ni moja ya miradi inayotekelezwa kwa msaada kutoka Serikali ya Japan kwa Nchi za Tanzania na Rwanda kupitia shirika lake la maendeleo la JICA.
Mradi huu kwa upande wa Tanzania umegharimu takribani kiasi cha TShs. 33,206,508,072.07 hadi kukamilika. Miradi mingine inayotekelezwa kwa kushirikiana na Serikali ya Japan kupitia JICA ni pamoja na ujenzi wa Barabara ya Arusha – Namanga, Iringa – Dodoma, Namtumbo – Kilimasera – Matemanga – Tunduru pamoja na barabara ya Masasi – Mangaka.
RAMANI KUONESHA DARAJA LA KISUMO LILIPOI

Leave A Comment

Copyright 2013 GlobalPublishers | All Rights Reserved

Saturday, 2 April 2016


Friday, 1 April 2016

Ronaldo vs Messi
Mapumziko ya lili mbalimbali kupisha mechi za kimataifa yamemalizika, sasa wachezaji wanarejea kwenye vilabu vyao kuendelea na majukumu yao. Mwishoni mwa juma hili zitapigwa mechi kibao kutoka ligi za mataifa mbalimbali, lakini akili, macho na masikio ya dunia nzima ni juu ya mchezo wa Barcelona dhidi ya Real Madri ‘El Clasico’ mchezo wa ligi ya Hispani maarufu kama La Liga.
Barcelona wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa mbele ya Madrid kwa pinti 10 wakiwa kileleni mwa msimamo wa ligi, mchezo huo utagubikwa na hisia juu ya kifo cha gwiji wa Barcelona Johan Cruyff aliyefariki juma lililopita na Barcelona wamepanga kutoa heshima zao kwa nyota huyo kwenye mchezo huo dhidi ya Madrid.
Siku hizi game ya El Clasico si vita kati ya Real Madrid dhidi ya Barcelona pekee bali na fursa kwa watu kuwalinganisha Cristinano Ronaldo na Lionel Messi ndani ya uwanja kutokana na upinzani wa ubora wa wachezaji hao nyota wa timu mbili tofauti.
Bila shaka hawa ndiyo wachezaji nyota kuwahikutokea katika vilabu hivi kuwa na upinzani mkubwa kwa wakati mmoja wakichezea vilabu vyao. Ni fursa nzuri ya kuwashuhudia Messi na Ronaldo wakicheza katika timu zenye upinzani mkubwa angalau mara mbili au zadi ndani ya msimu mmoja.
Ukweli ni kwamba, wawili hao wamepokezana tuzo ya Ballon d’Or katika kipindi cha miaka nane mfululizo.
Kuelekea mchezo wa El Clasico, ukilinganisha rekodi ya wachezaji hao kufunga magoli tangu Ronaldo alipojiunga na Madrid inafanana kwa kiasi kikubwa sana.
Ronaldo na Messi wanamagoli sawa wakiwa wacheza idadi sawa ya mechi, huku Messi akimzidi Ronaldo kwenye upande wa assists.
El Clasico tangu msimu wa 2009-10…
MESSI
24 idadi ya mechi alizocheza
15 idadi ya magoli aliyofunga
10 idadi ya assists alizotoa
CRISTIANO
24 idadi ya mechi alizocheza
15 idadi ya magoli aliyofunga
2 idadi ya assists alizotoa
Gazeti moja la Madrid linalofahamika kwa AS limelinganisha rekodi za Cristiano Ronaldo na Lionel Messi juu ya mchezo wa El Clasico, angalia ukurasa ma mbele wa gazeti hilo hapa chini.
Ronaldo vs Messi 1
AS linaripoti kwamba, hakuna mtu atakayebisha kwamba Ronaldo ni mchezaji wa mechi kubwa kwa mujibu wa takwimu walizozitoa.
Lakini kati ya michezo 24 ya El Clasico waliyokutana, Messi amefanikiwa kuisaidia Barcelona kushinda michezo 12, Ronaldo amefanya hivyo mara 6, huku michezo mingine 6 timu hizo zikitoka sare.
Ukichambua idadi ya magoli yao kwenye mchezo wa El Clasico, Ronaldo amefunga magoli 9 kwenye uwanja wa Nou Camp wakati Messi ametupia mara 10 akiwa Bernabeu. Hiyo inamaanisha wachezaji hao ni hatari kwenye mchezo huo bila kujali wapo kwenye uwanja gani.

Comments