This is featured post 1 title
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.
jiji la mwanza
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.

This is featured post 3 title
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, 31 March 2016


Mwenyekiti wa Kitongoji cha Bweya katika Kijiji cha Bweya mkoani Geita,
Augustine Katemi (42) ameuawa baada ya kufumaniwa akifanya mapenzi na
mke wa mtu vichakani.
Mwenyekiti huyo alifariki dunia papohapo
baada ya kudaiwa kushambuliwa kwa sime na mume wa mwanamke huyo, mkazi
wa Kijiji cha Luchili, Wilaya ya Buchosa mkoani Mwanza.
Tukio hilo lilitokea saa nne usiku Machi 28 baada ya marehemu kudaiwa kukutwa akifanya tendo la ndoa na Chausiku Isangula (32).
Hata
hivyo, alipoulizwa kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita,
Latson Mpojoli alisema hana za taarifa za tukio hilo na kuahidi kufuatilia.
Ilielezwa
kuwa Katemi aliuawa baada ya kushambuliwa kwa sime na kufa papohapo na
baada ya tukio hilo, mtuhumiwa anadaiwa kumshambulia mkewe kwa kutumia
sime hiyohiyo na kumsababishia majeraha makubwa sehemu mbalimbali za
mwili na amelazwa kwenye Kituo cha Afya cha Nzera.
Mtendaji wa
Serikali ya Kijiji cha Bweya, Samson Walwa alisema baada ya kutokea
tukio hilo wananchi waliendesha msako na kumtia mbaroni mtuhumiwa wakati
akijaribu kutoroka kuelekea Sengerema.
Walwa alisema mtuhumiwa
alikamatwa nyumbani kwa Edward Iswalala alipokuwa amefikia kwa siri
kutoka Luchili ili kufuatilia mwenendo wa mkewe ambaye anadaiwa kuwa
awali alimuaga kuwa anakwenda kumsalimia baba yake mzazi anayetibiwa kwa
mganga wa kienyeji.
“Inavyosemekana alikuwa akifuatilia
mienendo ya mke wake… sisi tulipomkamata tumemkabidhi Kituo cha Polisi
cha Nzera pamoja na nguo za marehemu (mwenyekiti) na zile za mkewe kwani
alipofanya mauaji hayo alizichukua nguzo zao hadi tulipomkata nazo,” alisema Walwa.
Mmoja
wa wananchi walioshuhudia tukio hilo, Jumanne Tole alisema, Chausiku
alimuaga mumewe kuwa alikuwa anakwenda kijiji cha Kalebezo kumsalimia
baba yake mzazi kwa waganga wa tiba asilia alikokuwa anatibiwa lakini
baada ya kufika na kumsalimia, alikwenda kwa kaka yake aitwaye
Ndagabwene Isangula huko Bweya alikofikwa na mkasa huo.
Alisema
kuna madai kuwa mtuhumiwa alifika kijijini hapo kwa siri akiwa amevaa
nguo na kofia zilizochakaa ili asifahamike wakati akifuatilia nyendo za
marehemu na mkewe na akafanikiwa ikidaiwa kwamba alikuwa na watu ambao
walikuwa wakimpatia taarifa hizo.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )


Kondakta wa daladala, Hamim Seif (42) mkazi wa Mwananyamala
Ujiji, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
akikabiliwa na shtaka la kutishia kumuua Rais John Magufuli kwa maneno.
Seif
alipandishwa kizimbani mahakamani hapo jana mchana na kusomewa shtaka
hilo na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kenneth Sekwao.
Mshtakiwa
huyo alikana shtaka hilo na Hakimu Mkazi, Hellen Liwa alisema kuwa
dhamana ya mshtakiwa huyo iko wazi na alitakiwa kuwa na wadhamini
wawili, kutoka taasisi ya Serikali inayotambulika, ambaye atasaini hati
ya dhamana ya Sh2 milioni.
Licha ya dhamana yake hiyo kuwa wazi,
mshtakiwa huyo alishindwa kukamilisha masharti hayo kwani baada ya
kusomewa mashtaka alipoulizwa kama alikuwa na wadhamini alishindwa
kuwapata.
Akimsomea shtaka linalomkabili, Wakili Sekwao alisema
kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Machi 10 mwaka huu katika baa ya
Soweto, Makumbusho wilayani Kinondoni kinyume cha kifungu cha 89 (2) (a)
na kifungu cha 35 cha Sheria ya Kanuni za Adhabu.
Wakili Sekwao
alisema akiwa katika baa hiyo, mshtakiwa alitishia kumuua Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Magufuli kwa maneno kwa njia ya
kujitoa mhanga.
“Kwa haya mambo anayoyafanya Rais Magufuli,
mimi nimo tayari kujilipua kwa kujitoa mhanga ili kumuangamiza,” alisema
Wakili Sekwao akimnukuu mshtakiwa huyo.
Hata hivyo, Wakili
Sekwao alisema upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na akaomba tarehe
nyingine kwa ajili ya kesi hiyo kutajwa.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka


Balozi
wa China nchini Tanzania Dkt. LU Youqing amefanya mazungumzo na Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira Mh. January
Makamba Ofisini kwa Waziri huyo Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam.
Katika
mazungumzo yao Balozi wa China amesema kuwa Serikali ya China inaamini
kwamba uchaguzi wa Zanzibar uliofanyika mwishoni wa wiki iliyopita
ulikuwa huru na haki.
Balozi
Youqing amesema kuwa Makamu wa Rais wa China ametuma salamu za pongezi
kwa Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein kwa kuchaguliwa kwake na kwa
watu wa Zanzibar kwa kuendesha uchaguzi huo katika misingi ya haki na
uhuru.
“Alikuwepo shuhuda wetu katika kushuhudia uchaguzi huo na alituambia kuwa ulikuwa wa haki na uhuru,” alisema Balozi huyo.
Katika
mazungumzo hayo Balozi Youqing alisema Serikali ya China itaendelea
kutoa misaada na kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwani huo ni wajibu wa
mataifa makubwa kwa nchi zinazoendelea.
Alimhakikishia
Mheshimiwa Makamba kwamba China ina mipango mingi ya ushirikiano na
Tanzania, ikiwemo kwenye sekta ya umeme na itaendelea kutoa ushirikiano
kwa Tanzania, ikiwemo kupitia makampuni ya China, ili kuhakikisha
malengo ya Tanzania kwenye sekta ya umeme yanatimia.
Kwa
upande wake, Mheshimiwa Makamba alimshukuru Balozi Youqing pamoja na
Serikali ya China kwa ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili.
“Ujumbe
na salamu ulizotoa leo umetupa faraja Watanzania. Urafiki baina ya nchi
zetu, na baina ya vyama vyetu vya CCM na CCP, ni wa muda mrefu, ni wa
majira yote, na umejengwa kwenye misingi ya kuheshimiana na hauna budi
kuendelezwa”, alisema Mheshimiwa Makamba.
Pia
Waziri Makamba na Balozi Youqing walikubaliana kutembelea Pemba na
Unguja kwa pamoja mwezi Aprili ili kukagua na kutengeneza miradi ya
maendeleo kati ya China na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Vilevile,
walikubaliana kuhusu kutengeneza mradi mkubwa wa ushirikiano kati ya
Serikali ya Jamhuri ya Muugano wa Tanzania na China kwenye teknolojia
zitakazosaidia kupunguza matumizi ya mkaa, hivyo kuhifadhi mazingira.
Waziri
Makamba pia amemueleza Balozi Youqing kuhusu hitaji na umuhimu wa
ushirikiano katika kuiwezesha Tanzania kumiliki teknolojia ya uzalishaji
wa nishati kwa kutumia taka ngumu zinazozagaa katika miji ya Tanzania
ambapo Balozi Youqing aliahidi kulifuatilia suala hilo.
IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI,
OFISI YA MAKAMU WA RAIS.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka


James Lembeli (Chadema ) Aangukia Pua Kesi ya Kupinga Ushindi wa Mbunge wa CCM Kahama
Mahakama
kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga leo imetupilia mbali maombi ya James
Lembeli wa CHADEMA ya kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa mbunge wa
Jimbo la Kahama Mjini wa Oktoba 25 2015, kwa madai kwamba taratibu
zilikiukwa.
Akisoma
hukumu iliyochukua saa tatu Jaji wa Mahakama hiyo Moses Mzuna amesema
ushahidi uliotolewa na upande wa Lembeli haukuwa na nguvu za kutosha
kuishawishi mahakama hiyo kutengua matokeo ya uchaguzi kwani sehemu
kubwa ni wa maneno.
Jaji
Mzuna amesema kitendo cha Lembeli kulalamikia vitendo vya rushwa
vidavyodaiwa kufanywa na mgombe wa kiti hicho kupitia Chama Cha
Mapinduzi (CCM), Jumanne Kishimba kushindwa kuvitolea taarifa kwenye
vyombo vya dola kimedhoofisha ushahidi na kuuwekea mashaka.
Kwa
upande wa mashahidi waliounga mkono kuwepo kwa vitendo vya rushwa Jaji
Mzuna amesema wameshindwa kujenga hoja kwa mlolongo unaofanana kiasi
kwamba wameonekana kana kwamba walikuwa na ushahidi wa kutengenezwa.
Akitoa
hukumu hiyo, Jaji Mzuba amefafanua kuwa madai ya unyanyasaji wa wafuasi
wake waliokamatwa na polisi katika hoteli ya Golden Rock na wengine
katika kata ya Ngogwa yamekosa nguvu kufuatia kukosekana kwa kielelezo
cha maandishi kinachoonesha kwamba walikuwa mawakala wake.
Mzuna
amesisitiza, sababu ya Lembeli kushindwa kupeleka malalamiko kwenye
kamati ya maadili ya uchaguzi iliyowekwa kisheria kwamba hakuwa na muda
wa kutosha haikubaliki kwa kuwa mpiga kura yeyote anayemuunga mkono
angeweza kulalamika.
Kufuatia
uamuzi huo wa mahakama kutupilia mbali maombi ya kutengua matokeo hayo
Lembeli amesema anaiheshimu mahakama, na kwamba atashauriana na wakili
wake kuona kama haki haikutendeka ili kukata rufaa.
Naye
Mbunge wa Jimbo la Kahama Mjini aliyekuwa mlalamikiwa namba moja katika
shauri hilo Kishimba alipohojiwa amesema Jaji ametenda haki kama
walivyotenda haki wananchi wa Kahama kwa kumpa kura za ushindi katika
uchaguzi wa oktoba 25,2015.
Shauri
hilo lilikuwa limevuta hisia za wananchi wa Kahama na kuhudhuria kwa
wingi leo kwenye hukumu yake huku makundi ya kisiasa yaani wana-CCM na
wana-CHADEMA yakijionesha wazi kwa kushangilia bila dalili zozote za
uvunjifu wa amani.
Subscribe to:
Posts (Atom)