Sunday, 23 August 2015

Kama kawaida uzinduzi wa kampeni za CCM kuelekea uchaguzi mkuu wa Urais, Ubunge na madiwani, uzinduzi wa CCM ambao ulipambwa na uwepo pia wa makada wa CCM kutoka katika tasnia ya filamu na wasanii wa bongofleva pia walikuwepo licha ya kutokana na ufinyu wa muda waliopata nafasi ya kuperform hadi sasa ni Peter Msechu, Yamoto Band na Diamond Platnumz sambamba na timu ya watu wake.
Kwa upande wa wasanii wa filamu na baadhi ya wasanii wa muziki wa bongofleva wao walipanda katika stage na kuimba wimbo wa taifa kwa pamoja.
Hizi ni picha zingine kutoka Jangawani
3X6A4082
3X6A4083
3X6A4103
3X6A4132
3X6A4143
3X6A4147
3X6A4148
3X6A4151
3X6A4153
3X6A4155
3X6A4157
3X6A4163
3X6A4165
3X6A4168
3X6A4174
3X6A4175
3X6A4177
3X6A4180
3X6A4183
3X6A4186
3X6A4187
3X6A4191
3X6A4197
3X6A4199
PAPO KWA PAPO zipate habari zote zinazonifikia za siasa muziki, michezo, maisha, Breaking news na nyingine kwa kujiunga hapa na mimi >>> Twitter Insta FB na nitakua nikikutumia kila ninachokipata pia usisahau kusubscribe YouTube kwa kubonyeza hapa >>>Videos

Klabu ya FC Barcelona imeshuka uwanjani kucheza mechi yake ya kwanza Ligi Kuu Hispania, FC Barcelona imeingia uwanjani kucheza na klabu ya Athletic Bilbao ikiwa ni wiki moja imepita toka ipokee kipigo kutoka kwa Athletic Bilbao katika mchezo wa Super Cup.
Generated by IJG JPEG Library
August 23 FC Barcelona imerudi kucheza mechi ya Ligi Kuu na Athletic Bilbao ila imefuta uteja wa kukosa ubingwa wa Super Cup ila katika mchezo wa Ligi Athletic Bilbao imekubali kipigo cha goli 1-0, goli pekee la dakika ya 54 kutoka kwa Luis Suarez liliwafanya FC Barcelona kuondoka na point 3 muhimu.
Generated by IJG JPEG Library
Generated by IJG JPEG Library
Generated by IJG JPEG Library
Generated by IJG JPEG Library
485015660
Generated by IJG JPEG Library
Generated by IJG JPEG Library

Tuesday, 18 August 2015


SIKU mbili baada ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), kumvua Ukamanda Mkuu, mwanasiasa mkongwe nchini, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru, uamuzi huo umepokewa tofauti na mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Edward Lowassa.
 
Tamko la UVCCM ambalo lilitolewa na Katibu Mkuu wa umoja huo,Sixtus Mapunda, lilisema wamefikia uamuzi huo kutokana na tabia, mwenendo wa Mzee Kingunge aliounesha hivi karibuni tofauti na maadili pamoja na taratibu za CCM.
 
Umoja huo ulipendekeza vikao vya CCM, kuuangangalia upya uanachama wake na kuchukua hatua kubwa zaidi.
 
Bw. Lowassa ambaye pia ni mgombea urais anayeviwakilisha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), alisema CCM itapata laana kama itaridhia kuondolewa kwa Mzee Kingunge.
 
Akiwahutubia mamia ya wafuasi wa UKAWA katika Viwanja vya Kibandamaiti, Mjini Zanzibar, jana ambako alikwenda kutambulishwa na kutafuta wadhamini, Bw. Lowassa alisema Mzee Kingunge ni mmoja kati ya wazee muhimu ndani ya CCM.
 
"Nasikitika sana kwa hatua kali alizochukuliwa Mzee Kingunge, kama isingekuwa yeye, CCM isingefika hapo ilipo, watapata laana," alisema.
 
Mapokezi yake
Lowassa aliwasili Zanzibar jana asubuhi akitokea jijini Mwanza kwandege ya kukodi akiwa na viongozi wengine wa UKAWA pamoja na mgombea mwenza, Bw. Juma Duni Haji.
 
Baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar, msafara huo ulipokewa na Katibu Mkuu wa CUF Taifa ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
 
Akihutubia mkutano huo, Lowassa aliwaambia Wazanzibar kuwa atahakikisha anazingatia taratibu za kisheria ili Masheikh wa Jumuiya ya Mihadhara ya Kiislamu (Uamsho) wanaoshikiliwa katika mahabusu jijini Dar es Salaam, wanapata haki zao.

Ahadi hiyo ya Lowassa ilisababisha umati huo kulipuka kwa furaha na vifijo huku ukimuita `Rais, Rais, Rais. 
 
Alisema kwa mara zote alizokwenda Zanzibar, hajawahi kushuhudia umati mkubwa kama aliouona jana. 
 
Lowassa alisema amekwenda Zanzibar kuomba dhamana ya wananchi na kurudia kauli yake kwamba anawania urais kwa kuwa anauchukia umaskini.

“Nataka kuwahakikishia Watanzania popote kwamba mabadiliko yataletwa na vyama vya upinzani. Nimetembea sehemu mbalimbali nimeona wananchi wanataka mabadadiliko ya uongozi,” alisema.

Kuhusu Katiba, alisema yeye ni muumini wa Serikali Tatu zitakazosaidia kuimarisha Muungano na kwamba msimamo wake huo aliouonyesha tangu miaka ya 90 wakati wa harakati za kundi la G55.

Alisema suala hilo litafafanuliwa vizuri wakati wa uzinduzi wa ilani ya uchaguzi Jumamosi wiki hii na wakati wa kampeni.

Hata hivyo, Lowassa alisema njia ya kuiondoa CCM madarakani, ni kwa kupiga kura na wananchi wajiandae pia kulinda kura.

Masheikh  waliofungwa
Alisema Masheikh mkoani Mwanza walimwomba azungumzie jambo hilo na kwamba atakachofanya atakapoingia madarakani, atazingatia taratibu za kisheria kufuatilia stahili zao.
Mpekuzi blog

MFANYABIASHARA wa duka la vipuri vya magari mjini Tarime mkoani Mara, Tumaini Jacob amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya akituhumiwa mauaji ya askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Anadaiwa kumuua askari huyo wa Kikosi cha Nyandoto, Roja Elias kwa kumpiga risasi tumboni wakati wakiwa baa moja mjini hapa baada ya kutokea ugomvi wa kunyang’anyana mwanamke ambaye ni mhudumu wa baa hiyo. Alisomewa mashitaka hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya Tarime, Marther Mpaze.

Mwendesha Mashitaka wa Polisi, George Lutonja alidai kuwa Jacob (45) Agosti 17 usiku saa 6 .30 wakati akiwa baa na Hoteli ya NK, kulitokea ugomvi kati yake na askari huyo.

Alidai katika ugomvi huo, Tumaini alichomoa bastola yake na kumpiga risasi Roja tumboni na kutokea mgongoni. Majeruhi huyo alikimbizwa Hospitali ya Wilaya ambapo hali yake ilizidi kuwa mbaya na kuhamishiwa Hospitali ya Rufaa Bugando ambapo mauti yalimkuta akipatiwa matibabu katika hospitali hiyo ya Bugando Mwanza.

Mtuhumiwa huyo Tumaini hakutakiwa kujibu lolote, kwani mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi za mauaji.
 
Mpekuzi blog
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )




 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetoa orodha ya majina 138 ya wanachama walioteuliwa na Kamati Kuu ya chama hicho kugombea ubunge wa majimbo ya uchaguzi.

Orodha ya majina hayo ya wanachama walioteuliwa kugombea ubunge katika majimbo hayo, imesainiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika kwa niaba ya Katibu Mkuu.
 
Taarifa imeeleza kuwa majimbo ambayo hayatakuwa kwenye orodha hiyo yatatolewa baada ya kukamilika kwa mashauriano ndani ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).
 
Katika mgawanyo wa UKAWA wa majimbo 253 Kati ya 265 ya kuwania ubunge, Chadema imeongoza kwa kupata majimbo 138 (54%), ikifuatiwa na CUF majimbo 99 (29% yakiwemo 49 ya Zanzibar), NCCR-Mageuzi majimbo 14 (5.5%) na NLD majimbo matatu (1.2%).
 
Ifuatayo ni orodha kamili ya majina ya wanachama wa Chadema walioteuliwa kugombea ubunge katika majimbo hayo.
 
Mara                        
  1. Rorya   STEVEN J OWAWA
  2. Tarime Mjini ESTHER N MATIKO
  3. Tarime Vijijini JOHN HECHE
  4. Musoma Vijijini ZAKARIA MBULA CHIRAGWILE
  5. Butiama        YUSUPH R KAZI
  6. Bunda Mjini  ESTHER BULAYA
  7. Mwibara  HARUN D CHIRIKO
  8. Musoma Mjini       VINCENT J NYERERE
  9. Bunda Vijijini  SULEIMAN DAUDI
Simiyu                      
  1. Bariadi        GODWIN SIMBA
  2. Maswa Magharibi ABDALA PATEL
  3. Maswa Mashariki SYLVESTER KASULUMBAYI
  4. Kisesa MASANJA MANANI
  5. Meatu          MESHACK OPULUKWA
  6. Itilima         MARTINE MAGILE
Shinyanga                
  1. Msalala             PAULO MALAIKA
  2. Kahama Mjini JAMES LEMBELI
  3. Kahama Vijijini (Ushetu) SIMON BUKAKIYE ISAYA
  4. Shinyanga Mjini PATROAS PASCHAL K
  5. Kishapu         FRED T MPENDAZOE
Mwanza                   
  1. Ukerewe JOSEPH MKUNDI
  2. Magu          KALWINZI NGONGOSEKE
  3. Nyamagana    EZEKIA D. WENJE
  4. Buchosa MARTINE KASWAHILI
  5. Sengerema HAMIS TABASAMU
  6. Ilemela         HIGHNESS KIWIA
  7. Misungwi LEONIDAS KONDELA
Geita                        
  1. Bukombe PROF. KULIKOYELA KAHIGI
  2. Busanda ALPHONCE C MAWAZO
  3. Nyang’wale GEORGE MABULA
  4. Chato          DR. BENEDICT LUKANIMA
  5. Mbogwe NICODEMUS H MAGANGA
Kagera                     
  1. Karagwe          PRINCE RWAZO
  2. Kyerwa          BENEDICT MTUNGIREHI
  3. Bukoba Mjini  WILFRED LWAKATARE
  4. Muleba Kaskazini  ANSBERT NGURUMO
  5. Muleba Kusini  ALISTIDES KASHASILA
  6. Biharamulo  DR. ANTHONY MBASSA
Mbeya                     
  1. Lupa         NJELU KASAKA
  2. Songwe          MPOKI MWANKUSYE
  3. Mbeya Mjini JOSEPH MBILINYI
  4. Kyela          ABRAHAM H MWANYAMAKI
  5. Rungwe         JOHN D MWAMBIGIJA
  6. Busokelo BONIPHACE A MWAMUKUSI
  7. Mbozi       PASCHAL HAONGA
  8. Momba        DAVID E SILINDE
  9. Mbeya Vijijini ADAM NZELA
  10. Tunduma FRANK MWAKAJOKA
  11. Vwawa FANUEL MKISI
Iringa                       
  1. Ismani         PATRICK OLE SOSOPI
  2. Kalenga        MUSSA L MDEDE
  3. Mufindi Kaskazini JUMANNE K MASONDA
  4. Iringa Mjini PETER MSIGWA
  5. Kilolo          BRIAN KIKOTI
  6. Mafinga Mjini WILLE MUNGAI
Njombe                    
  1. Njombe Kusini EMMANUEL MASONGA
  2. Lupembe (Njombe Kask) EDWIN E SWALE
  3. Wanging’ombe DISMAS A LUHWAGO
  4. Makete          JACKSON T MOGELA
  5. Ludewa           ATHROMEO MKINGA
  6. Makambako ORAPH MHEMA
Rukwa                     
  1. Nkasi Kusini ALFRED DANIEL SOTOKA
  2. Kwela          DANIEL NAFTAL NGOGO
  3. Nkasi Kaskazini KESSY SOUD
  4. Sumbawanga Mjini SADRICK MALILA
  5. Kalambo        VICTOR MATENI
Tanga                       
  1. Kilindi         JERADI K MREMA
  2. Muheza ERNEST MSINGWA
  3. Korogwe          AMANI H KIMEA
  4. Korogwe Vijijini EMMANUEL KIMEA
Kilimanjaro                       
  1. Rombo                   JOSEPH SELASIN
  2. Same Magharibi CHRISTOPHER S MBAJO
  3. Same Mashariki NAGENJWA KABOYOKA
  4. Moshi Mjini JAFARY P MICHAEL
  5. Hai          FREEMAN A MBOWE
  6. Siha         DR. GODWIN MOLLEL
Arusha                     
  1. Arumeru Mashariki JOSHUA NASSARI
  2. Arumeru Magharibi GIBSON MESIYEKI
  3. Arusha Mjini GODBLESS LEMA
  4. Longido        ONESMO OLE NANGOLE
  5. Monduli        JULIUS KALANGA
  6. Karatu         WILLE QAMBALO
  7. Ngorongoro ELIAS NGORISA
Manyara                  
  1. Simanjiro JAMES KINYASI OLE MILLYA
  2. Mbulu Vijijini MIKEL PETRO AWEDA
  3. Hanang          MAGOMA RASHID DERICK
  4. Babati Mjini PAULINE P GEKUL
  5. Babati Vijijini LAURENT SURUMBU TARRA
  6. Kiteto        KIDAWA ATHUMANI IYAVU
  7. Mbulu Mjini PAULO HERMAN SULLE
Dar es Salaam                  
  1. Ubungo        SAED KUBENEA
  2. Kawe        HALIMA JAMES MDEE
  3. Ukonga          MWITA MWIKWABE WAITARA
  4. Ilala         MUSLIM HASSANALI HEIDERALI
  5. Kibamba JOHN JOHN MNYIKA
Pwani                       
  1. Chalinze MATHAYO TM. TORONGEY
  2. Kibaha Mjini MICHAEL PAUL MTALY
  3. Kibaha Vijijini EDITHA BABBEIYA
Morogoro                
  1. Mikumi         JOSEPH HAULE
  2. Morogoro Kusini DAVID LUKAGINGIRA
  3. Kilombero PETER E LIJUALIKALI
  4. Mlimba        SUZAN L. KIWANGA
  5. Mvomero OSWALD MLAY
  6. Ulanga Magharibi ALPHONCE MBASSA
  7. Ulanga Mashariki PANCRAS KONGOLI
  8. Morogoro Mjini MARCOSSY ALBANIE
Dodoma                   
  1. Kongwa             ESAU NGOMBEI
  2. Dodoma Mjini SINGO BENSON KIGAILA
  3. Bahi         MATHIAS LYAMUNDA
  4. Chilonwa JOHN CHOGONGO
Singida                     
  1. Iramba Magharibi JESCA KISHOA
  2. Iramba Mash(Mkalama) OSCAR KAPALALE
  3. Singida kaskazini DAVID DJUMBE
  4. Singida Mashariki TUNDU A LISSU
  5. Singida Magharibi MARCO ALLUTE
  6. Manyoni Magharibi LUPAA DONALD
  7. Manyoni Mashariki ALLUTE EMMANUEL
Tabora                     
  1. Nzega Mjini CHARLES MABULA
  2. Igunga        NG’WIGULU KUBE
  3. Urambo         SAMWELI NTAKAMLENGA
  4. Ulyankulu DEUS KITAPANDYA NGERERE
  5. Sikonge       SAID NKUMBA
  6. Manonga ALLY KHALFANI NGUZO
Katavi                      
  1. Mpanda Mjini JONAS KALINDE
  2. Mpanda Vijijini MUSSA MASANJA
  3. Katavi          GEORGE SAMBWE
  4. Nsimbo GERALD KITABU
  5. Kavuu         LAURENT SENGA MANGWESHI
Kigoma                    
  1. Kigoma Kaskazini DR. YARED FUBUSA
  2. Kigoma Mjini          DANIEL LUMENYELA
Ruvuma                   
  1. Peramiho         ELASMO MWINGIRA
  2. Mbinga Magharibi/Nyasa CUTHBERT S. NGWATA
  3. Mbinga/Mbinga Vijijini EDWIN B AKITANDA
  4. Songea Mjini        JOSEPH FUIME
  5. Madaba EDSON MBOGORO
Mpekuzi blog
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )